Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipatia nafasi na mimi niweze kuchangia hoja iliyoko hapa mezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu wote waliosema kwamba kwa kweli elimu yetu inaendelea kushuka sana na elimu hii imeshuka kwa sababu kadhaa; na pia tumeshuhudia walimu wakuu wakifukuzwa kazi, walimu wakuu wakishushwa vyeo kwa sababu shule zao zimefanya vibaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii tunaita kwenye taaluma ya management services tunaita blame culture. Blame culture ni utamaduni ambao unatafuta mchawi. Jambo limeharibika unamtafuta mchawi wa kumbebesha huo mzigo kwamba yeye ndiyo amesababisha bila kuangalia ni sababu zipi zimefanya hizi shule zisiweze kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ziko nyingi, sababu moja ya kwanza ambayo naiona mimi kubwa sana ni mfumo ambao kila Waziri anayekuja anakuja na ajenda yake. Tulianza kuona shule zile za mchepuo agriculture na biashara zikaondolewa, akaja mwingine kaondoa michezo, kaja mwingine ka-introduce GPA, amekuja wa sasa amerudisha division, curricular zinabadilishwa kabla walimu hawajazifahamu vizuri, zimebadilishwa. Kwa hiyo kuna mambo mengi ambayo yanasababisha shule zetu zisiweze kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi napendekeza kwamba sasa tuiombe Serikali iweke mfumo ambao utazuia Mawaziri wa Elimu kubadilisha mitaala, kubadilisha mifumo ya elimu bila ya kupata majadiliano na tukakubaliana elimu yetu iwe vipi na isiwe rahisi kwa Waziri tu anaamka asubuhi, anabadilisha mitaala au anabadilisha mfumo wa elimu, hilo ndiyo pendekezo langu la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuungana na marais wale wawili Mheshimiwa Mkapa na Mheshimiwa Kikwete waliosema tunahitaji mjadala mpana kuhusu elimu yetu kwa sababu kwa kweli elimu yetu haiko vizuri. Kwa hiyo, nashauri Serikali huo mjadala uweze kufanyika ili tuweze kuamua elimu yetu tunayoitaka ipi ambayo itatupeleka kwenye Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri pia Serikali juu ya mazingira ya kufundishia kwamba si mazuri, tukianzia na walimu. Walimu wote tunajua malimbikizo yao hawalipwi, hawapandishwi vyeo na hata mazingira ya kufundisha hayapo mazuri, msongamano wa wanafunzi madarasani, hizo ni changamoto kubwa ambazo zinaathiri elimu yetu hapa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, motisha ya walimu; tukiangalia statistics za BEST zinasema walimu 35 tu ndio ambao wana motisha, wakati walimu 63 hawana motisha ya kufanya kazi. Kwa hiyo, ili tuweze kupata elimu bora kwa kweli rasilimali watu ya walimu ingekuwa ndicho kitu cha kwanza kabisa kwa ajili ya kuwapa motisha waweze kupata moyo, waweze kufundisha, waweze kuwekwa kwenye mazingira mazuri na elimu yetu itaweza kupanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuangalia mnyororo wa elimu kwa ajili ya Tanzania ya Viwanda. Nimeangalia taarifa ya Mheshimiwa Waziri na bado sijaona kwa mfano katika admission au usajili wa wanafunzi hasa katika sayansi sijaona ni pool gani kubwa ambayo tumesema tutawasajili au tutaweka kwenye vyuo waweze kukidhi yale matakwa ya Tanzania ya Viwanda. Nimeona kwenye VETA tunaongeza wanafunzi 200,000 mpaka 250,000 na nikawa najiuliza, je, hawa 200,000 mpaka 250,000 ndio ambao tumewa-target kwa ajili ya Tanzania yetu ya viwanda? Maana ni muhimu kuinyambua na kujua ni skills zipi ambazo tutazihitaji kwa ajili ya shughuli zote za viwanda kwa Tanzania yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia pia katika taarifa ya Mheshimiwa Mpango ambaye alitaja baadhi ya madaktari sijui ma-engineer na nini, lakini tunahitaji kunyambua na kujua. Kwa mfano tungeweza kuona katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri ni pool gani kubwa ambayo tutakwenda kuisomesha kwa ajili ya Tanzania ya viwanda. Bado sijaona na ninapendekeza sana Mheshimiwa Waziri ajipange kusudi hata ile pool ya sayansi na teknolojia ikidhi yale mahitaji ya Tanzania yetu ya viwanda, kwa sababu bila hivyo tutajikuta tumekuwa na viwanda, tumekuwa sijui na Stieglers, tumekuwa na reli lakini hatuna pool kubwa ya wataalam…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)