Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia katika Wizara hii. Kwanza kabisa niweze kutoa pole kwa Mheshimiwa Heche kupotelewa na ndugu yake, Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naenda moja kwa moja katika kuchangia na naomba nianze na maneno yafuatayo ya aliyekuwa Rais wa Marekani Abraham Lincoln ambaye alishawahi kusema naomba ninukuu; “The philosophy of the school room in one generation will be the philosophy of the government in the next.” Ana maana kwamba falsafa ya elimu inayotolewa darasani kwenye kizazi cha leo ndiyo itakayokuwa hatma ya Serikali ya kesho. Tunaona jinsi ambavyo elimu yetu inakwenda ICU. Elimu yetu haiko katika muafaka kabisa, watoto wengi wanamaliza wakiwa hawana ujuzi, maarifa na ubunifu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona katika ripoti ya Kamati jinsi ambavyo shule binafsi zinaongoza kuanzia mwaka 2016. Mwaka 2016/2017 shule 10 bora zote za kitaifa zilikuwa za private na watoto bora wote wa kitaifa walikuwa wanatoka shule za private na ukiangalia kidato cha pili hivyo hivyo. Hii maana yake nini, maana yake kwamba kama kungekuwa hakuna shule zisizo za kiserikali division one, two na three zingekuwa hazipo kabisa. Sasa tufanye nini? Mimi naumia sana ninavyosikia kwamba mnazuia kukaririsha katika shule za private. Shule za private wanakaririsha kwa sababu wanataka wapate vijana wenye ujuzi, wenye maarifa, wasiende kama taburarasa, waende wakiwa wanaelewa nini wanachokifanya kwa kila kidato, kuanzia darasa la nne, saba, form one, two mpaka form four, sisi tunataka walingane, ama mnataka kutekeleza ule usemi wa Mheshimiwa Rais aliyosema kwamba matajiri wanataka waishi kama maskini. Kwa sababu wanapeleka watoto kule ili waweze kujikwamua katika elimu ninyi mnataka walingane wote tupate ma-zero, hili halikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika suala la Bodi ya Walimu ambayo itakuwa ni independent board. Naomba hili lifanyike, Mheshimiwa Waziri unapokuja utuambie ni lini Bodi hii itaanza, kwa sababu itawianisha na kupima shule za private zinakaguliwa na kupewa masharti lukuki, lakini shule za Serikali hakuna masharti yoyote yanayotolewa. Iwe haina choo, iwe ina choo ni kuendelea, hii haikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakwenda sasa katika suala la walimu. Walimu wamekata tamaa, asilimia 37.8 ya walimu ndio wenye hamasa ya kufundisha, lakini asilimia 60 ndio hawana hamasa kabisa ya kufundisha. Ina maana hawa walimu kama mlivyosema kauli zile zinazotolewa mara kwa mara kwamba asiyetaka kazi aache.

Sasa walimu wameacha kazi wamebaki na utumishi. Mheshimiwa Waziri walimu wameacha kazi, wako na utumishi. Wamekata tamaa kwa sababu hawana motisha kama ambavyo wanapewa shule za private, walimu hawa unakuta anafanya bora liende, shule hakuna discipline, mwalimu anaenda anasoma anaweza akawa anafundisha au asifundishe, haya yanatokea Mheshimiwa Waziri. Kwa hiyo, tukuombe Mheshimiwa uliangalie kwa jicho la ndani kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la lugha ya kufundishia; kiingereza na kiswahili. Wamezungumza wenzangu hapa lugha za kufundishia ni jambo muhimu sana katika elimu. Usipokuwa na lugha ambayo umeamua ifundishiwe tunakuwa na mchanganyiko. Tumeona katika shule za private wanafundisha kwa Kingereza. Wanaaanzia darasa la tatu kiingereza wanakwenda nacho na shule za government ni Kiswahili lakini darasa la nne wanakutana na mtihani wa pamoja, sijui kusudi na maudhui yake mnataka wapate nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakienda kufika darasa la saba wanamaliza, wakienda sekondari hawa waliotoka shule za government wamesoma Kiswahili, wanaenda kukutana na lugha ya Kiingereza wanapata taabu, matokeo yake unakuta wanaanza kuibia. Kwa hiyo, kunakuwa na kazi kubwa sana watoto wanaibia wanasema wanapiga chabo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa toka form one mpaka form four, anakwenda form five mpaka form six anapiga chabo; unatarajia huyu mwanafunzi akija kupata kazi atapiga chabo wapi sasa wakati anafanya kazi? Kwa hiyo, hii ni changamoto Mheshimiwa Waziri uangalie kama

hakuna lugha maalum ya kufundishia muone jinsi mtakavyofanya. Mimi ni mwalimu by profession, lugha ya kiingereza unakuta zile phonetics watoto wadogo wanasoma kwa sauti, unajua sauti ndiyo inaingia na inakaa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)