Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Watanzania wote wana haki ya kushtaki ama kushtakiwa isipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jambo linaloshangaza, mwanafunzi yupo kwenye kiwango cha elimu ya juu anafanya masomo yake ya degree ya kwanza university anashtakiwa, prospectus ya chuo yaani kanuni ya uongozaji wa chuo inazuia mwanafunzi yule asiendelee na masomo, ni jambo la kushangaza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya chuo kikuu ni tertiary education na tafsiri yake ni third level education, ni elimu ya ngazi ya tatu. Amepita elimu ya msingi, elimu ya sekondari, university education level ni elimu ya watu wazima. Wanaosoma pale sio lazima wawe vijana, wengine ni watu wazima; wengine wanashtaki na wengine wanashtakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Elimu, jambo la mwanafunzi Abdul Nondo kuwa ameshtakiwa na chuo kikamsimamisha masomo, it is contrary to human rights, very contrary. Kama prospectus ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inasema hivyo, prospectus ya namna hiyo haifai na sheria hiyo inapaswa ifutwe. Ni sheria isiyokwenda na wakati lakini pia inanyima na inazuia haki za binadamu lakini pia inakwenda kinyume na Katiba yetu. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaoa fursa ya mtu kushtaki na kushtakiwa. Sasa hivi ni kweli wanafunzi wote waliopo vyuo vikuu aliyekuwa na kesi mahakamani ni Abdul Nondo peke yake? Hivi ni kweli? Kwa hiyo, kama sheria za chuo zinasema hivyo, sheria hii hebu ifuteni, inawatia aibu, vinginevyo mtuambie kwamba jambo hili mmelichukulia kisiasa.

T A A R I F A . . .

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na taarifa yake nimeipokea kwa msisitizo kabisa.

Jambo hili linakichafua Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, tuseme ukweli, to be sincerely, hadhi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inashuka kwa sababu mnataka kuwaingiza kwenye siasa. Hata hapo UDSM tukifanya leo sensa ya wanafunzi wangapi wenye kesi mahakamani hawatapungua hata wanafunzi 20, 30 lakini aliyeonekana mwenye makosa ni mmoja tu, this is quite unfair. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kama ingekuwa vyuo vikuu vinafanya mtihani wa pamoja kama ilivyokuwa elimu ya sekondari, vyuo vikuu vya Serikali vingekuwa vinashindwa kama ambavyo shule za sekondari za Serikali zinashindwa dhidi ya shule binafsi. Pamoja na mambo mengine yanayochangia ni hizi kanuni na sheria zilizopo kwenye vyuo, hizi prospectus za chuo Mheshimiwa Waziri jaribuni kuzipitia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambapo mimi nimesoma pale. Hivi unakwendaje kwenye chuo unakuta kuna mchepuo au fani wanafunzi wanasoma, chuo cha Serikali miaka mitatu wanahitimu, wakienda Serikalini wanaambiwa hii haitambuliki, yaani chuo cha Serikali lakini mtu amehitimu anaambiwa haitambuliki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere watu wamesoma faculties zaidi ya tatu, lakini mwisho wa siku wanaambiwa hizi hazitambuliki. Sasa chuo cha Serikali inakuwaje wanasomesha kitu ambacho hakitambuliki? Jambo hili na lenyewe ni la aibu sana. Mheshimiwa Waziri nitakuja kukupa orodha ya hizo faculties ambazo wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere wamezisoma, leo mtaani huko wakiomba ajira wanaambiwa kwamba hizi hazipo kwenye system ya Lawson na huwezi kuajiriwa, ni jambo la aibu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu la Mchinga lina shule nyingi za sekondari. Shule ya Sekondari ya Mchinga sasa ni kongwe inafanya vizuri sana, ni miongoni mwa shule zinazofanya vizuri, tumeomba muipandishe hadhi iwe shule ya A-Level. Naomba sasa Mheshimiwa Waziri mwaka huu uje unithibitishie kwamba ile shule mtaitengea fedha. Shida yetu sisi ni mabweni tu, mkitupatia mabweni shule itapanda hadhi, ina walimu wa kutosha, ina walimu wengi wenye degree, ina wanafunzi wengi, lakini pia catchment area yake ina shule nyingi ambazo wanaweza wakai-feed shule ya sekondari Mchinga ikaweza kuwa shule ya A-Level na ikaweza kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni jambo la kuhamisha walimu kuwatoa shule za sekondari kuwapeleka shule za msingi. Jambo hili sio baya kwamba kama dhamira ni hiyo sio mbaya, tatizo ni namna linavyotekelezwa. Leo mwalimu aliyesomea kufundisha wanafunzi wa sekondari anakwenda kupelekwa akafundishe wanafunzi wa darasa la kwanza, darasa la pili bila kumfanyia orientation, jambo hili haliwezi kuwa na tija. Walimu wenyewe wana frustrations za kutosha, information yenyewe haijatolewa vizuri, namna ilivyochukuliwa na Wakurugenzi kule chini Mkurugenzi huyu analitekeleza kivyake, Mkurugenzi mwingine anatekeleza kivyake, wengine wamepewa fedha ya uhamisho…

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.