Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo. Lakini pia niwapongeze Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yao nzima kwa kazi nzuri na kubwa wanayoifanya, ningependa kushauri katika baadhi ya maeneo ambapo ushauri huu ukizingatiwa naamini kwamba tunaweza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta hii ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi tunahitaji kuwekeza zaidi katika vocation training yaani katika masuala ya ufundi wa hasa katika shule zetu za VETA. Mwaka 2014 Serikali ilileta hoja Bungeni kwa dharura kwamba ilikuwa inahitaji kutumia zile fedha za Skills Development Levy (SDL) ile four percent; asilimia mbili iende kwa ajili ya kusaidia kutoa mikopo kwa wanafunzi kipindi hicho hali ilikuwa ni mbaya na kweli ilisaidia Watanzania wengi. Sasa kwa ajili ya urejeshwaji wa ile mikopo ni mzuri sana na unakusanya fedha nyingi, naomba ile two percent ambayo inaenda kwenye Bodi ya Mikopo ya Skills Development Levy irudi sasa na ile asilimia zote nne ziweze kutumika kwenye VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, VETA yetu bado tunaenda na mfumo ule wa zamani teknolojia ya zamani, leo hii kwa sera yetu ya viwanda tunahitaji kuwa na mafundi mchundo (technicians) ambapo leo hii wengi wenye degree tunao, lakini hao ngazi ya technicians hatuna kabisa yaani ni wachache mno. Sasa ni vizuri VETA zote zikaboreshwa kwanza kwa vifaa na vifaa vingi vinatakiwa tubadilishe pia mfumo uendane na masuala ya IT, leo hii hata fundi wa umeme wa nyumbani, fundi wa magari suala la kupima na ile teknolojia ya zamani imepitwa, leo hii ni lazima wajue namna ya kufanya programming, kwenye magari yote ya kisasa lazima unaenda pale unatumia diagnostic equipment ambapo VETA zetu hazifundishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme wa majumbani kote siku hizi unaona kuna sensors, watu kama hawajui ku-program hata akipata ufundi pale VETA akitoka mtaani hatapata kazi kwa sababu ni masuala ya kutumia IT. Kwa hiyo, ni vizuri tuwe na transformation kubwa, mabadaliko makubwa kwenye VETA kwenda na wakati na njia pekee ya kwenda na wakati na kuwekeza zaidi na kuwekeza zaidi kunahitaji fedha kwa hiyo, ile asilimia mbili ambayo inakwenda Bodi ya Mikopo tuirudishe ije huku na VETA ikifanya vizuri Watanzania wengi watakuwa wanaweza kujiajiri kwa sababu Serikali haina uwezo wa kuajiri watu wote ambao wanahitimu vyuo. Sasa ni vizuri tukahakikisha kwamba VETA zetu zote zinapata, ile fedha na irudishwe na ziboreshwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ile programu ya entrepreneurship iweze kurudishwa, mafundi wetu ambao wamejifunza wenyewe kwa kufanya practicals, yaani kujiunga na maeneo mbalimbali na mafundi wenye uzoefu sasa waweze kufanya programu ndogo ndogo za muda mfupi ili na wao sasa wahitimu na wawe na vyeti na wanaweza kujiendeleza kusoma. Kwa hiyo, suala la VETA ni muhimu sana.

Mheshimiwa, lakini lingine lilikuwa ni suala la kuhakikisha kwamba tunakuwa na mfumo wa kuhakikisha masuala ya utafiti yanapata fedha, kwa sababu masuala ya sayansi na tekonolojia yako katika Wizara hii, mimi nilikuwa napendekeza ule mfumo, kwa mfano, ile pesa ya TTMS ambayo ilikuwa COSTECH, leo hii ile fedha imeondolewa kwa sababu COSTECH imehama Wizara sasa haipo kule kwenye wizara nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba tuangalie na vyanzo vingine kwasababu ahadi huko ilikuwa tupate one percent ya bajeti nzima kwenda kwenye utafiti lakini ikashindikana, tukaahidiwa kwamba itakuwa bilioni thelathini; lakini hata hiyo kwenye bilioni thelathini fedha iliyokwenda kwa maximum ni bilioni kumi na mbili. Na kwenye utafiti mbali na tuseme upande kilimo tu ambao unahitaji zaidi ya bilioni thelathini kwa haraka lakini utafiti wa mambo mengine yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo suala la kupatiwa fedha kwenye mfuko wa utafiti yaani COSTECH ni muhimu sasa Serikali wakati tunakuja kwenye finance bill tuwe na vyanzo mbadala na vyanzo vingine ili tuhakikishe kwamba tunafanyaje ili angalau kwa mwaka waweze kupata si chini ya bilioni mia moja ili tuweze kusaidiana katika masuala mbalimbai ya utafiti; na bila utafiti hakuana kitu ambacho kitaweza kuendelea ndani ya nchi hii. Kwa hiyo ninaomba wakati Waziri anapokuja basi watueleze kwamba wamepanga vipi, kwamba suala la COSTECH kupatiwa fedha za kutosha ili tuweze kwenda kwenye utafiti mbalimbali tunaweza kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine lilikuwa binafsi naipongeza Serikali kwa kuanzisha mfumo huu wa kuboresha zile shule za zamani; na nilikuwa pia naomba muanze kuifikiria Shule ya Sekondari Gidas. Ni shule ambayo ilikuwa ni middle school enzi hizo, imejengwa 1947 nayo muifikirie. Lakini pia Wizara mnapopanga fedha kwenda kwenye shule mbalimbali za kuboresha muangalie Wilaya zenye shule nyingi na idai kubwa ya shule, isifanane na Wilaya ambazo zina shule chache yaani uwiano kati ya Wilaya ambazo zina shule nyingi na zile ambazo zina shule chache pia fedha ziende kwa uwiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nilikuwa napenda Serikali iliangalie, niipongeze Serikali kwa kukubali kuwa na PPP kwenye mambo ya vyuo. Chuo cha kwanza cha PPP kiko Babati, Mamire pale. Ni mpango mzuri ambapo kwa kushirikiana na wadau mbaimbali wa private sector ambapo Mheshimiwa Jenista aliweza kuja kuzindua kile chuo mwaka juzi, nampongeza kwa hilo, alichukua mammuzi magumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo mngeweza kujifunza kutokana na Mamire, nina uhakika kabisa hivi vyuo vingine vyote ambavyo Serikali hamuwezi kufanya pekeenu, hebu mjifunze kutokana na hii PPP mnaweza kupata partners kwenye vyuo vyote, kama tunavyofanya kwenye afya, kwa kushirikiana na taasisi za dini. Kama mnaona hiyo moja ni nzuri, hiyo ya Mamire basi inaweza kuwa ya mfano. Vyuo vingine vyote vya ualimu na vyuo vikuu vikaingia kwenye partnership ili vizweze kusaidiwa na Serikali kwa namna ya kuboresha vyuo hivyo na namna ya kuboresha elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ambalo ni muhimu sana; nilikuwa naomba Serikali ifikirie, Chuo Kikuu cha Sokoine, Chuo pekee cha Kilimo hapa Tanzania, nilikuwa naomba kiondoke kweye Wizara ya Elimu kirudi Wizara ya Kilimo kwa sababu Wizara ya Elimu wanafanyakazi nzuri. Wao vyuo vyote ni sawa kwao, watoto kwao ni sawa lakini ikipelekwa Kilimo kwa sababu ndio wenye uhitaji na wahitimu wa pale wote ndiyo wanakwenda kwenye sekta hiyo ya kilimo, mifugo, uvuvi na masuala ya misitu, wao wataionea umuhimu na watakuwa wanaisimamia kwa ukaribu zaidi.

Kwa hiyo, ningeomba ninyi mbaki kwenye sera lakini Chuo Kikuu hiki cha Sokoine mkirudishe Wizara ya Kilimo ili Wizara iweze kusimamia vizuri na mtaona kwamba ubora wa elimu pale na namna ya kusimamia na namna ya kufanikisha matokeo yatakuwa ni bora zaidi kwa sababu wao ndiyo walengwa na wao watakuwa na moyo zaidi wa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)