Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi jioni ya leo na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunipa uhai na afya mpaka leo muda nipo humu Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri anayofanya na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia lakini ina mapungufu katika baadhi ya sekta zake, nianze na NECTA. Kwa kipindi kirefu Baraza la Mitihani limekuwa likitunga mtihani wa darasa la saba kwa kutumia aina moja tu ya maswali yaani multiple choice. Sasa unapotunga mtihani kwa kutumia multiple choice peke ina maana hau- provide room kwa huyu mwanafunzi kuweza kujieleza kwa zaidi. Vilevile mtihani wa hivyo haupimi hizi skills zingine za language kama vile kuandika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ili hawa watoto wetu waweze kufanya vizuri na kwenye mitihani ijayo ni lazima basi mitihani itungwe kwa ku-mix other types of questions ili mwanafunzi aweze kuwa na nafasi ya kujieleza zaidi. Kwa sababu sasa hivi mwanafunzi anafanya mtihani kwa kutumia aina moja tu ya maswali, swali la kwanza mpaka la 50 na anafanya tu betting kwa sababu anahisi tu kwamba hili litakuwa jibu na kuna wengine wana bahati anaweza akajibu lile jibu na likawa jibu sahihi kweli. Kwa hiyo, naomba wizara iangalie utungaji wa maswali haya ili kuweza kupima other skills of language kwa hawa wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tuangalie namna gani wanavyojibu hii mitihani ya darasa la saba. Wanafunzi wetu wanajibu hii mitihani kwa kutumia karatasi za OMR. Serikali imetumia hizo karatasi kwa ajili ya kujirahisishia wao usahihishaji, lakini hawampimi huyu mwanafunzi namna gani anaweza kuandika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi karatasi hazimpi mwanafunzi uwezo wa kuandika zaidi ya kuweka shading pale kwenye lile jibu. Unakuta mtoto anafaulu kwenda form one ilhali hajui kuandika chochote lakini amefaulu, this is shame, naomba Serikali iliangalie suala hili kwa undani ili watoto wetu waweze kufanya mitihani yao vizuri na waweze kufaulu kwa kiwango kinachotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi inakuwaje hadi mtihani wa hisabati unakuwa na multiple choice, mtihani kuwa na multiple choice ina maana unamsaidia huyu mwanafunzi kuelekea jibu. Mwanafunzi akokotoe mwenyewe, naomba sana wizara tuache mtihani wa hisabati uwe wa kawaida na usiwe na multiple choice.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni kuhusu Loans Board. Loans Board wanafanya kazi nzuri sana, watoto wengi wa kimaskini wameweza kwenda vyuo vikuu na kutimiza ndoto zao. Hata hivyo, hii Loans Board imekuwa ni mwiba sana kwa hawa wafanyakazi hususan Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua wazi kabisa mwaka 2016 mlifanya mabadiliko ya sheria kutoka kulipa asilimia nane mpaka 15. Jamani, huyu mtumishi wa Tanzania ana makato mengi sana yanayomkabili, ana income tax, ana PSPF, ana makato ya NSSF, ana makato ya CWT, makato mengi kiasi kwamba mshahara unabakia mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo sheria imekiuka ile thamani ya kubakia mshahara 1/3 imekiuka, kwa hiyo, inampa mtihani mkubwa sana huyu mtumishi kufanya kazi kwa mashaka na stress nyingi. Kwa hiyo naomba basi kama hii sheria ipo na sheria sio maandishi ya Qur-an au Msahafu kwamba hayawezi kufanyiwa marekebisho. Naomba basi sheria kama ipo iletwe kwa sababu ni sheria kandamizi, inawakandamiza watu wengi sana hata sisi inatukandamiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba hii sheria iletwe humu au Serikali sasa itoe tamko wale watu waliokumbwa na hii sheria ina maana loans beneficiaries before 2016 basi walipe ile ile asilimia nane na hawa ambao wako baada ya 2016 walipe kwa hiyo asilimia 15, itakuwa inawasaidia hawa wafanyakazi. Kwa kweli wanafanya kazi kwa stress nyingi maisha yamekuwa ni magumu vitu vimekuwa bei juu wanashindwa kufanya kazi kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)