Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sekunde tano nimpongeze sana Waziri na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri wanayofanya lakini harakaharaka niende kwenye Wilaya ya Makete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri ambayo Wizara inafanya niombe sana Mheshimiwa Waziri kwenye shule ya sekondari ya Iwawa majengo yamechakaa sana na barua zimekuja kwako ambapo karibu shilingi bilioni 2.6 zinahitajika ili kuweka sawa shule ile. Ikumbukwe shule ile ilikuwa ya kwanza kimkoa wa Njombe na ni shule ya Serikali, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia shule ya sekondari ya Lupila, ni A-Level, chondechonde uikumbuke. Shule ya sekondari ya Kipagalo uikumbuke na shule ya sekondari ya Ikuo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo niseme tu kwa ufupi. Tumekuwa tukijadili sana kuhusu elimu na ubora wa elimu. Kabla sijachangia, nihoji maswali mawili au matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bora ni ile ambayo inatoa majibu ya matatizo tuliyonayo katika nchi au katika jamii, ndiyo elimu bora na siyo vinginevyo. Swali linakuja, je, elimu tuliyonayo leo kutoka darasa la kwanza mpaka vyuo vikuu inafasili matatizo ya Watanzania? Maana nguvu ya Watanzania ni kilimo, uvuvi na ufugaji lakini toka darasa la kwanza mpaka vyuo vikuu hakuna mahali ambapo elimu hiyo inatiliwa mkazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa lugha nyingine hata kama wanafunzi wa kidato cha nne wote Tanzania wangekuwa daraja la kwanza kwa ufaulu, kidato cha sita wakapata daraja la kwanza na vyuo vikuu wakapata daraja la kwanza, kwa maana ya first class, utawapeleka wapi? What next? Hawawezi kujiajiri na hawawezi kuajiriwa. Kwa hiyo, hoja leo si suala la quality education as far as our education system is concerned, ni issue ya relevance of education system. Elimu tuliyonayo ni irrelevant, kwa nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mwanafunzi wa kidato cha nne hakuna anachoweza kufanya, kidato cha sita hakuna anachoweza kufanya, hata tukimpa wa shahada ya kwanza hakuna anachoweza kufanya. Ndiyo maana ninapandekeza lazima tufanye overhaul of education system. Tutengeneze masomo kuanzia darasa la kwanza mpaka hilo la saba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninashauri darasa la kwanza liende mpaka darasa la nane, kwa nini? Kwa sababu masomo ya darasa la sita na la saba kwa kiasi kikubwa ndiyo yanayosomwa form one na form two, isipokuwa ni lugha inabadilika. Tukienda darasa la kwanza mpaka la nane tuende sasa darasa la tisa mpaka la kumi na mbili inaishia hapo, tunaondoa five na six. Sababu ya kuondoa five na six ni kwa sababu hakuna uhusiano wa masomo ya kidato cha tano na sita na degree yoyote ndani ya nchi yetu. Ukimchukua leo mwanafunzi wa kidato cha nne ukampeleka kuanza degree ya kwanza atafanya vizuri tu, mkitaka jaribuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili haraka haraka ni la lugha. Jamani Mheshimiwa Mwenyekiti na Wabunge wenzangu ni vizuri mfahamu kiswahili, kiingereza, kireno, kijerumani ni lugha ambazo tumeamua kuzifuata kwa sababu ya kutawaliwa. Hakuna mtu ambaye amezaliwa
kabila lake wanaongea kiswahili au kiingereza ama kireno ama kifaransa. Kama mwalimu Nyerere na wenzake wangeamua Tanzania tuongee Kingereza tungekuwa tunaongea kiingereza hivi hivi na tungekuwa tunajivunia kwamba ni lugha yetu. Kwa hiyo, kiswahili siyo lugha ya kwetu ni lugha iliyotokana na kutawaliwa na waarabu, sawasawa na kiingereza, kireno na kifaransa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali la kujiuliza, je, hawa watawala wetu walifanya uchaguzi wa maana? Kwa sababu kiswahili as of today nchi hazizidi nne zinazoongea Kiswahili kwa ufasaha lakini kiingereza Afrika peke yake ni nchi 25, kihispaniola ni nchi zaidi ya hizo. Kwa hiyo, ni wajibu wetu sasa kufikiri kwa usahihi kwamba walimu wanaomaliza vyuo vikuu wapewe dossier ya kufundisha primary schools ili walimu wenye shahada waanzie shule za msingi kufundisha Kiingereza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Makete, baba yangu ni Mahanji mama yangu ni Mkinga, kwa hiyo, naongea kwa ufasaha kikinga na kimahanji. Naongea kwa ufasaha pia kimagoma, kiwanji, kibena, kikisi kwa sababu ndio makabila yanayopatikana Makete. Je, kwa kujua kiswahili ambayo ni lugha mpya, nimeweza kuharibu lugha yangu ya baba na mama? The answer is no. Kiswahili hakijaharibu kimahanji, kikinga, kimagoma changu na Wabena, Wasukuma na Wachaga vivyohivyo. Kwa hiyo, kujua kiingereza hakuharibu kiswahili chako bali kinakuongezea nguvu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nilikuwa kwenye mkutano pale Dubai, mimi ni Financial Advicer. Pale Dubai kuna madereva 12,000 kati ya hao wanaoendesha tax, 2,700 ni Wakenya, sababu wanajua lugha. Sisi kwetu tunawa- barred, tunawa-deter madereva wetu kwa sababu ya lugha, lugha is a problem. Kwa dunia ya sasa ukiwa conversant na lugha nyingi ni mtaji.

Mheshimiwa Mwneyekiti, kwa hiyo, niombe sana mliangalie hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka niende kwenye elimu ya juu. Naomba sana fedha zinazopelekwa COSTECH kwa maana ya Tume ya Sayansi zioanishwe na shahada za uzamili na uzamivu kwenye vyuo vikuu. Kwa lugha nyingine Serikali i-identify maeneo ambayo wanataka kufanya utafiti COSTECH wa execute hiyo programu, vyuo vikuu vya private na vya Serikali viombe ili mtu akifanya utafiti wake anaisaidia Serikali kupata majibu ya maeneo wanayotaka lakini wakati huohuo unaongeza idadi ya shahada za uzamivu na uzamili ili twende kwa pamoja. Tukifanya hivyo, tutaongeza sana idadi ya wanazuoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa TCU, tusipoangalia itakuwa ni tume ya chuo fulani kimoja kwa nature ya waajiriwa wake. Niombe sana viongozi wa TCU ni lazima wawe na weledi hiyo moja na wawe wamesoma vyuo mbalimbali ili akiwa pale asitizame chuo kimoja. Pili, awe pia amefundisha vyuo mbalimbali ili pia awe na weledi wa anachotaka kusukuma vinginevyo itakuwa ni Tume ya Vyuo Vikuu lakini kwa kweli inayokuwa dictated na chuo kimoja, itakuwa ni mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo TCU waongoze weledi na hasa kwenye kutambua watu wanaomaliza shahada kwenye nchi zilizoendelea. Watoto wetu wanapomaliza vyuo vikuu vya nje…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.