Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza kuongelea kuhusu upungufu wa walimu wa sayansi. Suala hili limekuwa ni changamoto katika maeneo mengi nchini kwani mpaka sasa idadi ya wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi ni tofauti na wanafunzi wanaosoma masomo ya sanaa. Hivyo, Wizara ichukue jambo hili na kulifanyia kazi ili tuweze kumaliza tatizo hilo la walimu wa sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni nizungumzie shule binafsi. Kulingana na mchango wa shule binafsi katika Serikali suala hili liangaliwe kwa kupunguza kero zile zinazowafanya watu wa shule binafsi wavunjike moyo ili kuboresha elimu yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni suala la elimu bure. Naomba suala hili liangaliwe upya kwani kuna changamoto ambazo zinaikabili sekta ya elimu ikiwemo kutopeleka pesa shuleni jambo ambalo linawakwamisha kufanya mambo ya msingi ambayo wamejipangia kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne ni kuhusu madai ya walimu. Ili tuwe na matokeo chanya ni lazima kuwe na mazingira rafiki kwa walimu pamoja na wanafunzi. Madai ya walimu yamekuwa ya muda mrefu ambayo kwa sasa yanawaathiri wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, walimu wa sekondari kupelekwa kufundisha shule za msingi. Suala hili halijawahi kutokea katika nchi yetu na linaweza kuathiri wanafunzi kwani wanafunzi wa shule ya msingi wanahitaji kujengewa msingi na walimu wenye level hiyo.

Suala la sita ni upungufu wa vitabu. Kulingana na umuhimu wa vitabu katika kuboresha ufaulu wa wanafunzi, Wizara iweke kipaumbele kununua vitabu na vitabu viandaliwe kwa ubora ili wanafunzi wapewe elimu sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, saba, kiandaliwe chombo maalum kwa ajili ya kusimamia elimu ili kuleta tija. Jambo

hili likisimamiwa vyema litaleta matokeo chanya kwa Wizara ya Elimu na itakuwa rahisi kumaliza matatizo yanayoikabili Wizara kwani watakuwa wanatembelea na kujua matatizo.