Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na Sera ya Viwanda na Biashara, nashauri Serikali ifufue na kuimarisha Vyuo vya VETA katika mambo yafuatayo:-

(i) Ifundishe mafundi mchundo ili kukidhi mahitaji ya viwanda vitakavyoanza;

(ii) Mafunzo maalum ya ujasiriamali yatolewe; ma

(iii) Chuo cha VETA Tabora kipelekewe vifaa vya kisasa kwani ni chuo kikubwa; kipelekewe walimu wa kutosha na gari la mafunzo ya driving na wanafunzi wanaomaliza mafunzo wapewe mitaji ili wajikwamue kimaisha na kuendeleza ujuzi wao (cherehani, vifaa vya ujenzi na kadhalika).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu rushwa, nashauri mitaala ianzie kidato cha kwanza mpaka cha nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upungufu wa walimu, nashauri Serikali iangalie kujaza nafasi kwenye shule zenye upungufu mkubwa hasa vijijini wa walimu wa masomo ya sayansi na hesabu, kukamilisha maabara nchini na kuwapa mikataba walimu wa masomo ya sayansi na hesabu waliostaafu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukarabati wa shule kongwe, niipongeze Serikali kwa kukarabati shule kongwe hapa nchini. Naishukuru kwa kuona umuhimu wake kama vile Shule ya Wasichana Tabora lakini bado kuna kero kubwa ya uzio kwenye shule zote za Mkoa wa Tabora ambazo ni Tabora Girls, Tabora Boys, Milambo na Kazima. Niiombe Serikali kuongeza bajeti kwenye shule hizo ili tukamilishe maana ya ukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni ya watu mbalimbali wanaoidai Serikali. Niiombe Serikali tulipe madai ya wazabuni, walimu na wakufunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule ya wasiojiweza/ wasioona. Niombe wapewe walimu wa kutosha katika ngazi ya shule za sekondari na vyuo.