Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nampongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako pamoja na Naibu Waziri Mheshimiwa Ole Nasha kwa kazi nzuri wanayofanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili wanafunzi wawe na ufaulu wa kiwango cha juu ni lazima Serikali ifanye yafuatayo:-

(i) Iboreshe na iwaongezee walimu mishahara na posho;

(ii) Iwapandishe madaraja wale waliofundisha zaidi ya miaka mitatu;

(iii) Ijenge madarasa ya kutosha na maktaba pamoja na maabara katika shule za sekondari na shule za msingi;

(iv) Ijenge nyumba bora za walimu na ni muhimu ziwe na umeme ili walimu waweze kuandaa maazimio na maandalio ya kazi kwa masomo ambayo watayafundisha siku inayofuata darasani;

(v) Isajili shule za awali (chekechea) ili kuweza kutambulika kisheria. Pia itengeneze mitaala kwa shule hizi na ziwe na miundombinu inayolingana na uhitaji wa watoto hao wa chekechea;

(vi) Ipeleke mashuleni vitabu vya kiada na ziada kwa wakati;

(vii) Itengeneze mitaala ya sekondari inayomuandaa kijana/mwanafunzi kujiajiri. Mfano kuwe na masomo ya needle work, cookery, wood work, metal work, fine arts na kadhalika kama ilivyokuwa zamani katika shule mfano Morogoro sekondari.

(viii) Iwe na mtaala wa michezo ili kuweza kukuza vipaji kwa wanafunzi wetu;

(ix) Ijenge ofisi za walimu na kuweka samani katika ofisi hizo ili walimu waweze kuzitumia katika shughuli za kiofisi;

(x) Ijenge vyoo vya walimu na wanafunzi katika shule zetu. Mfano, katika Shule ya Msingi Yombo Dovya iliyopo Kata ya Makangarawe, Wilaya ya Temeke hakuna matundu ya vyoo vya kutosha; na

(xi) Iandae angalau mlo mmoja kwa siku katika shule zetu ili kusaidia wanafunzi waweze kuhamasika kuhudhuria masomo. Pia kupata mlo ambao utawasaidia kuwa na afya njema na kuelewa vyema masomo yao maana mwanafunzi akiwa na njaa hafundishiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho namtakia Waziri wa Elimu na Naibu wake afya njema na Mwenyezi Mungu awape umri mrefu ili waweze kuyatekeleza majukumu yao ya kila siku.