Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, naomba kutoa mchango katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi vyuo vikuu vyote duniani huwa na kazi tatu ambazo ni training, research na consultancy. Research grants hutolewa kwenye vyuo vikuu kwa kuzingatia ubora wa research zinazofanyika na publications kwenye Four Stars Journal. Utaratibu huu huhamasisha vyuo kufanya tafiti bora na kuchapisha makala mbalimbali kwenye journals za Kimataifa. Nashauri Serikali kuangalia uwezekano wa kutumia utaratibu huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya zilizo nyingi hapa nchini kuna upungufu mkubwa wa walimu katika shule za msingi na sekondari pia katika Wilaya ya Misenyi tuna upungufu wa walimu 750 katika shule za msingi. Pamoja na utaratibu huu mkubwa, utaratibu unaotumika kugawa walimu wachache wanaopatikana hauko sawa. Kwa mfano, mwaka 2014 katika Wilaya tatu Mkoani Kagera zilizopangiwa zaidi ya walimu 700 kila Wilaya huku Wilaya nyingine zikipangiwa chini ya walimu 10, jambo hili siyo zuri lazima uwekwe utaratibu mzuri wa kugawa vizuri walimu katika shule za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la wakaguzi kutotembelea shule za msingi. Kwa mfano, shule ya msingi Kajunguti iliyo Wilaya ya Misenyi kwa muda mrefu Wakaguzi hawajatembelea shule hiyo. Aidha, shule hiyo ina walimu wanne tu na walimu hao hawakai kwenye kata hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Gera kina changamoto nyingi. Hivi karibuni Mheshimiwa Waziri wa Elimu alitembelea Chuo hicho na kutoa maelekezo mbalimbali ya kusaidia kuboresha ukarabati wa chuo hicho pamoja na maelekezo hayo mazuri hakuna utekelezaji wowote uliofanyika hasa kuhusiana na VETA kutakiwa kutumia fedha zao kukarabati baadhi ya majengo ya chuo hicho, baada ya VETA kutumia vibaya milioni 100 kukarabati baadhi ya majengo chini ya kiwango. Naomba Wizara ifuatilie suala hili kwa karibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.