Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia. Pamoja na pongezi hizo ninapenda kuiomba Wizara, Wilaya yetu ya Mbogwe ipo katika mchakato wa kuanzisha kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari ya Mbogwe, je, Serikali haioni kwamba muda umefika sasa kuhakikisha kwamba shule ya sekondari Mbogwe inafunguliwa rasmi hasa baada ya ujenzi wa mabweni na bwalo tayari vimekamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo ni kutokuwepo kwa chanzo cha uhakika wa maji, niiombe Serikali itoe kipaumbele cha kuifungua shule hii ya Mbogwe haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya elimu ni muhimu kuanzishwa kwa vyuo vya ufundi katika kila Wilaya, niiombe Serikali yetu ihakikishe chuo cha ufundi kinaanzishwa katika Wilaya yetu ya Mbogwe, pia tunaiomba Serikali itoe kipaumbele katika kuhakikisha kuna kata tunazojitahidi kukamilisha shule zao za kata za Wanda, Isebya na Ngemo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamejitahidi sana katika kuchangia nguvu zao katika kujenga madarasa na maabara pamoja na nyumba za walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi ni changamoto kubwa. Kuna upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi, niiombe Serikali itupatie ili hatimaye vyuo vya ufundi viweze kupata wanafunzi wazuri wa kuweza kujiunga na vyuo hivi vya ufundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha naiomba Serikali kuhakikisha inatusaidia kupatiwa fedha zaidi ili kuhakikisha nyumba za walimu pamoja na vifaa vya kujifunzia ikiwa ni pamoja na vitabu na vifaa vya maabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa mkakati wake wa kutoa elimu bure kwa elimu ya msingi hadi sekondari. Naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri.