Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasikitika kuona hadi sasa Serikali haijapeleka vitabu vya kiada vya darasa la nne licha ya kwamba wanafunzi hawa wanajiandaa na mitihani ya Taifa ya darasa la nne. Je, Serikali haioni kama inatengeneza mazingira ya kuwafelisha wanafunzi kwa kutopeleka vitabu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017 shule zilizoibuka bora 100 za Serikali ni sita tu kati ya hizo. Kwa miaka mingi sasa shule za watu binafsi zimekuwa zikifanya vizuri ukilinganisha na shule za Serikali. Utafiti unaonesha kwamba matokeo mazuri ya shule binafsi unatokana na motisha kwa walimu, mishahara mizuri kuliko ile ya Serikali na mazingira bora ya kufanyia kazi. Tangu mwaka 2014 Serikali haijawahi kupandisha mishahara kwa watumishi wakiwepo walimu. Hivyo walimu wengi wa shule za umma wamekosa moral ya kufanya kazi kwa bidii. Litakuwa jambo jema kama Serikali itajifunza mbinu za kufundishia na kujifunzia kutoka shule binafsi. Pia mishahara ingeboreshwa kwa watumishi wa umma ili walimu waliokata tamaa warudishe moral.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Songwe hauna chuo cha VETA hivyo naishauri Serikali ijenge chuo katika mkoa huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.