Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

HE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Nampongeza Waziri na Naibu Waziri wake kwa uchapakazi wao zaidi kwa hotuba iliyoletwa kwetu imeandaliwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Nkasi kuna zaidi ya sekondari 22 zinazofanya kazi lakini zote zinakabiliwa na changamoto mbalimbali, za upande wa Nkasi Kusini jimboni kwangu zina shida sana za walimu wa sayansi. Naomba Serikali ituletee walimu hawa kila wanapopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, majengo ya maabara bado hayajakamilika katika shule nyingi zikiwemo shule za sekondari za Milundikwa, Chala, Ninde Wampembe, Sintali, Kala, Kipande, Nkundi, Kate na Ntuchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maalum kabisa shule ya sekondari ya Milundikwa iliyohamishwa toka makazi ilipokuwa na kupelekwa Kasu ina shida ya kukosa hata nyumba moja ya mwalimu na ukizingatia ni shule ya boarding kwa kidato cha tano na sita. Watoto wa kike wanakaa peke yao mabwenini, hawachungwi kabisa na matron wakati wa usiku wakipata shida. Naomba nyumba hata moja tu. Vilevile miundombinu yake yote iliyobaki hakuna mabweni ya watoto wa kiume, lakini madarasa bado hayatoshelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule zote za kata hazifanyiwi ukarabati zikijengwa. Serikali haizipatii fedha ya ukarabati zinaharibika tena, upo umuhimu kuzipa fedha ya ukarabati. Tunaomba Wizara iwe inatembelea shule hizi za pembezoni kuona hali mbaya iliyoko huko ili waweze kubuni namna ya kuwapa motisha watumishi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu waliohamishwa kwenye shule ya sekondari ya Milundikwa iliyotwaliwa na Jeshi kwa maelekezo ya Serikali hawajalipwa haki zao. Naomba walipwe ili waendelee kuchapa kazi kwa moyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Chuo cha Maendeleo ya Wananchi cha Chala naiomba Serikali kutofanya ukarabati wa chuo kwenye majengo yake ya sasa kwani si mali yetu na Askofu wa Jimbo la Sumbawanga ambaye ndiye mwenye majengo ametoa ilani ya kufukuza chuo ili ayatumie majengo yake. Wananchi kupitia vikao vya WDC tumeamua kutoa majengo ya iliyokuwa iwe shule ya sekondari Isoma ambayo ina majengo mengi yanayotosha kuanzia na ukarabati ukifanyika pale itakuwa ni sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za sekondari nyingi hazina miundombinu ya maji na mfumo wa maji machafu. Shule zote nilizotaja hazina maji ya uhakika na hivyo miundombinu ya maji ya usafi wa vyoo na matumizi yake ni changamoto mfano Nkundi secondary school.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali mtekeleze yote niliyoyachangia hapo juu.