Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu kwa kasi kubwa inakumbwa na ongezeko la idadi ya watu. Hali hii kwa njia moja au nyingine itaathiri utendaji wa Wizara ya Elimu. Mheshimiwa Waziri ameliona hili na amejipanga vipi katika kuwahudumia wananchi hawa kwa kuongeza idadi ya walimu na mahitaji mengine ya lazima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mahitaji ya viwanda, nchi yetu inaelekea kuwa Taifa la viwanda. Viwanda vinahitaji rasilimali watu watakaofanya kazi yenye ufanisi na zenye tija. Kwa hiyo, Wizara ya Elimu ni lazima iandae mikakati kwenye vyuo vyetu vikuu ili kuwawezesha vijana wetu wanaohitimu mafunzo yao waweze kufanya kazi katika viwanda kwa ufanisi na tija ili kutimiza ndoto ya nchi yetu kufikia maendeleo waliyojiwekea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu changamoto za elimu ya juu, kama Mheshimiwa Waziri alivyosema katika hotuba yake (page 42) kwamba elimu ya juu ni nguzo muhimu ya kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake ya maendeleo kwa kuzalisha rasilimali watu. Naomba Mheshimiwa Waziri atueleze katika vyuo vyetu kuna wahadhiri wa kutosha? Iwapo ni wachache, je, hawana manyanyaso kwa wanafunzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anafahamu kwamba mafunzo ya baadhi ya shahada uzamili hapa nchini si chini ya miaka minne na mafunzo hayo hayo ni chini ya miaka miwili kwa nje ya nchi? Namuomba Mheshimiwa Waziri afahamu kwamba mafunzo ya shahada ya uzamivu katika vyuo vyetu yana usumbufu. Unaweza kusoma mpaka ukajukuu bado hujapata kuhitimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwaombe wahadhiri wetu wa vyuo vikuu wafanye wajibu wao kama walivyotumwa wa kuzalisha rasilimali watu kwa maendeleo ya Taifa letu. Wahadhiri wawe tayari kurithisha ujuzi wao kwa vizazi vipya na kufanya hivyo ndiyo taifa letu litakaposonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.