Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (The Mwalimu Nyerere Memorial Academy) kilichopo Kigamboni Dar es Salaam kuna faculty (fani) ambazo watu wamesomea lakini huko kwenye soko la ajira wanaambiwa faculty hizo hazitambuliki katika mfumo wa ajira (caurdon). Nakutajia faculty hizo ni Politics And Management of Social Development na Gender and Development (GD).

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali naomba sana ufafanuzi wa jambo hili kwa kuwa ni kilio cha wahitimu wengi ambao hivi sasa wapo mtaani zaidi ya miaka mitatu bila ya kupata ajira Serikalini. Mheshimiwa Waziri, jambo hili ni aibu kwa Serikali kwa kuwa chuo hiki ni cha Serikali na miongoni mwa vyuo vikongwe hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kubwa ni kwamba chuo hiki hakijakamilika kwa jengo la hosteli la ghorofa tatu, ambalo limeanza kujengwa zaidi ya mika mitano sasa. Jengo hili lilikusudiwa kuwa hostel ya wanafunzi wa shahada ya pili (Masters Degree Students Hostel) mwaka huu nimeona mmetenga shilingi bilioni moja kwa ajili ya Development Project. Sasa je, hii bilioni moja ndiyo inakwenda hapo au sehemu nyingine tofauti?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali, namuomba sana Mheshimiwa Waziri, tupatieni fedha ya mabweni katika Shule ya Sekondari Mchinga ili shule iweze kupandishwa hadhi kuwa ya A-Level. Shule ni kubwa, ipo sehemu nzuri na imezungukwa na shule nyingi za sekondari hivyo catchment area yake ni kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba Mheshimiwa Waziri, nitumie lugha ya sanifu ya kiswahili, chonde chonde, itazameni Mchinga sekondari, muipatie mabweni ili shule iweze kupanda hadhi hiyo. Shukrani sana.