Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. WILLY Q. QAMBALO: Mheahimiwa Mwenyekiti, nianze na eneo la Vyuo vya Ufundi (VETA). Tanzania imedhamiria kuwa na Chuo cha VETA katika kila Wilaya na hili ni jambo jema. Wilaya ya Karatu kwa kushirikiana na wadau wake wa maendeleo wamejenga Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) na majengo ya msingi yamekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto tuliyonayo Karatu ni msajili wa chuo hicho na hatimaye uendeshaji wake. Tunashukuru tumepata usajili wa muda miezi sita na tayari fani mbili zimeanza. Naomba Serikali kutupatia usajili wa kudumu na kisera kusaidia Halmashauri ya Wilaya ya Karatu kuendesha Chuo hicho kwa kutupatia walimu na vifaa vya ufundishaji. Tunao upungufu mkubwa sana wa watumishi. Wilaya ya Karatu ina upungufu wa walimu wa msingi 546 na sekondari 66. Idadi hii ya upungufu ni kubwa mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule ya msingi Endamaghang Wilayani Karatu ni maalumu ya bweni kwa watoto wa jamii ya Wahadzabe na Wabarbaig ambao kwao bado mwamko wa elimu ni mdogo sana. Shule hiyo ina changamoto na upungufu mwingi sana. Shule hiyo haina umeme japo nguzo zimepita hapo. Pia walimu hawatoshi kabisa, nyumba za walimu hazipo na mabweni kukosa vifaa kama magodoro na mashuka. Wahudumu mfano wahunzi na wapishi hawatoshi na hawapati mafao yao kwa muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu wetu nchini wanazo changamoto nyingi sana ikiwemo mishahara midogo, kupandishwa madaraja na pia nyumba zao. Naishauri Serikali kuondoa changamoto hizi ili watumishi katika sekta ya elimu wapate moyo wa kufanya kazi kwa bidii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamejitahidi kujenga maabara na changamoto kubwa iliyopo sasa ni watumishi wa kada ya laboratory technicians. Serikali ipeleke watumishi wa ngazi hii Wilaya ya Karatu. Tumejitahidi sana kujenga shule za sekondari 31 kwenye kata 14. Serikali sasa itupe upendeleo wa kukamilisha maabara katika shule 18 ili hatimaye watoto wetu wapate kujifunza kwa vitendo.