Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kwa maandishi hoja hii muhimu ya elimu. Kwanza nianze na motivation kwa walimu. Serikali imeshindwa kutoa motisha kwa walimu wa shule za sekondari na msingi ndiyo maana ufaulu umeshuka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu madai ya msingi ya walimu kupandishwa madaraja, kulipwa arreas (malimbikizo), likizo, uhamisho na kadhalika. Madai hayo yote yasiposhughulikiwa kwa wakati hali ya ufaulu katika shule za Serikali itaendelea kuwa mbaya na kamwe hazitaweza kushindana na shule binafsi ambazo kwa sasa zimechukuliwa role ya Serikali badala ya shule za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni uhamisho walimu wa arts kwenda shule za msingi. Tumeshuhudia walimu wengi wakiripotiwa kwenye vyombo vya habari kwamba wamejinyonga na wengine kufa kwa msongo wa mawazo. Kuendelea kuwashusha walimu kutoka shule za sekondari kwenda shule za msingi pasipokuwaandaa kisaikolojia (counseling) bado wanajiona kama ni demotion kwao na inawavuruga moyo. Inahitajika motivation ya aina yake kwa walimu hao ili waweze ku-cope na mazingira mapya wanayoenda kukutana nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifikirie namna ya ku-motivate shule binafsi ambazo zinatoa aibu Taifa hili. Shule binafsi zimesaidia kupandisha kiwango cha ufaulu kwa kiasi kikubwa kwenye Taifa hili na hii imefanya wazazi wengi sasa wanasomesha watoto kwenye shule za private badala ya kupeleka Kenya, Uganda na Malawi kama ilivyokuwa zamani, hivyo pesa zilizokwenda nje ya nchi sasa zinabaki hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali isipunguze masharti katika shule hizi hasa kuwapunguzia gharama zilizokuwa muhimu ili kuziwezesha shule hizi kuendelea kufanya vizuri? Badala ya Serikali kupambana na shule za private kuweka masharti magumu, sasa wazipe fursa na kuwajengea uwezo na mazingira rafiki ili waendelee kuwekeza kwenye elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure bado haijaisaidia nchi hii. Sasa hivi imekuwa ni malalamiko kila kona, bado Serikali imeshindwa kupeleka huduma muhimu kwa wanafunzi katika shule za msingi; chakula mashuleni hamna. Moja ya sababu zilizotolewa na Taarifa ya Kamati ya Wizara ya Elimu ni kukosekana kwa chakula mashuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure wanafunzi wana njaa; elimu bure wanafunzi hawana madawati shuleni, wazazi bado wanachangishwa, elimu bure bado wazazi wanalipia gharama za ulinzi, maji, umeme na kununua vitabu. Hiyo siyo elimu bure, ni lazima Seriklai ingefuta ghrama zifuatazo; chakula, ulinzi, vitabu mashuleni na kadhalika.