Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Wizara hii sana kwa mambo mazuri sana waliyowatendea wakazi wa Jimbo langu, kama vile ujenzi wa nyumba vya madarasa primary na secondary. Wizara hii imesaidia sana ujenzi wa sekondari ya Makongoro kwa mabweni na nyumba. Shule hii ina kidato cha kwanza na cha sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba shilingi milioni 72 kumalizia ujenzi wa bwalo la Chalanda, watoto wanalia nje, mvua na jua lao. Sekondari ya Mekomariro tunajenga bweni, tunaomba samani za bweni (vitanda, meza na kadhalika).

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni sekondari za Nyamangita, Salama Rihingo na Chamriho, Nyamangutu. Naomba ujenzi wa maabara. Kwa upande wa Salama, jengo la maabara lipo katika kata, tunaomba fedha za kumalizia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chamriho na Mihingo watoto wanasafiri kilometa 17 kutoka eneo la shule ya sekondari. Tunaomba Wizara mtusaidie maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri pamoja na Kamati ya Huduma za Jamii, akiwepo Naibu Katibu Wizara ya TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, nilitoa taarifa ya kubomoka na kuanguka kwa shule za msingi Sarawe na Stephen Wasira ambapo watoto wawili walifariki.

Mhshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi kutoa msaada wa dharura kwa shule hizi mbili. Naomba ahadi hii itekelezwe, kwani mwakilishi na Serikali (Mkuu wa Mkoa) kwa niaba ya Serikali na Wizara ya Elimu waliahidi kusaidia kutoa msaada wa dharura.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo sugu ambalo liko kimya, tatizo la mikopo ya watumishi na hasa walimu ambao ndio wengi. Walimu wanakopa kuliko uwezo wao, hakuna limit ingawa zipo sheria za mikopo, lakini hazifuatwi. Naomba Wizara ifanye tathmini ya kuhusu jambo hili. Tafuteni udhibiti wa namna mikopo ya mabenki katika eneo la walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ya wanafunzi iwe kwa wanachuo toka Diploma hadi Chuo Kikuu na mikopo iwe kwa ngazi zote au mwaka wa kwanza hadi wa tatu bila kujali hakuna mwaka wa kwanza au wa pili au wa tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.