Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri sana inayofanywa na Waziri wa Elimu, lakini kuna baadhi ya wasaidizi wake wanamwangusha sana. Kwa mfano, VETA Mikumi imefanya jambo baya sana kwa wananchi wa Jimbo la Mikumi, kwani VETA-Mikumi wakishirikiana na Chama cha Mapinduzi (CCM) wameanzisha utaratibu mbaya sana na unawanyima haki wananchi wanyonge kwa sababu wananchi wanaambiwa ili mtoto aweze kupokelewa kuingia VETA - Mikumi ni lazima awe na kadi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamekasirika sana na wako mbioni kuandamana kudai haki yao ya msingi ya kujiunga na Chuo hiko cha VETA – Mikumi, kwani mpaka sasa fomu zote za VETA zinagawiwa na makada wa Chama cha Mapinduzi na kuwanyima fursa wananchi wengine wa vyama vingine na hata wale wasiokuwa na vyama. Maana tunavyojua, Vyuo vya VETA siyo mali ya CCM bali ni vyuo vya umma na vinatakiwa kutoa fursa sawa kwa wananchi wote bila kuangalia itikadi zao, dini wala makabila yao. Cha msingi wawe wamekidhi vigezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina shaka na utendaji wa kazi wa Mheshimiwa Waziri kwa wananchi. Naomba sana atakapokuja kuhitimisha atoe karipio kali kabisa kwa VETA - Mikumi na wasitishe zoezi wanalolifanya mara moja na watupe majibu ni nani aliyewatuma kunyanyasa wananchi kwa kuwabagua kwa vyama vyao? Mwisho wale waliohusika na zoezi hili, wawajibishwe mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waziri hatatoa majibu ya kueleweka, nakusudia kushika shilingi ya mshahara wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.