Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nchi yetu bado inawahitaji wamiliki wa shule binafsi kama wadau wa elimu, ni vyema yafuatayo yakazamwa upya. Kodi nyingi zinazomwelemea mmiliki wa shule ambazo hatima yake ni kuwazidishia mzigo wazazi katika ada, ni vyema kodi nyingi hizi zikaondolewa kama ilivyo katika sekta ya afya. Serikali iendelee kudhibiti ubora wa elimu. Hoja ya shule binafsi kujitengenezea udhibiti isikubaliwe kwa kuwa imekuwa ikitumika vibaya kwa baadhi ya shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni upungufu wa walimu wa sayansi. Naiomba Serikali iendelee kutafuta suluhu ya upungufu wa walimu wa sayansi na naomba kuishauri Serikali kuruhusu wahitimu wa kada za sayansi za vyuo mfano, engineering na kadhalika ambao wapo mtaani kuajiriwa kama walimu kwa kuwa masomo yanafanana.