Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata fursa hii ya kuchangia kwa maandishi na nitajikita katika kilimo. Nashauri Serikali ijikite katika kutoa elimu juu ya uzalishaji wa mazao bora ya kilimo. Kwa mfano, Mkoa wangu wa Iringa una Kiwanda cha Nyanya chini ya mwekezaji kiitwacho DARSH kwa ajili ya kusindika nyanya. Iringa huzalisha karibu zaidi ya 50% ya nyanya inayozalishwa Tanzania lakini kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa uhakika wa nyanya. Wakulima wamekuwa wakilima nyanya zisizokidhi ubora unaotakiwa kiwandani kwa kukosa elimu ya kilimo bora cha nyanya.
Pia wakulima hawa hawajaandaliwa kwa kilimo hicho kwani wengi wao hulima kienyeji. Mahitaji ya kiwanda ni zaidi ya tani 200 kwa siku ambapo mara nyingi hazipatikani na wengine husafirisha kwenda Mkoa wa Dar es Salaam. Hivyo, uzalishaji wa kiwanda hicho hauna tija kwa kuwa wakulima hawajaandaliwa. Nashauri Serikali iwaandae wakulima kuzalisha kwa ubora na uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu au changamoto nyingine ni gharama ya mbegu. Mfano, hybrid seed (Eden na Asila) gramu 30 kwa ekari moja ni Sh. 210,000. Ni gharama kwa wakulima wetu walio wengi, nazungumzia (hot culture). Vile vile hakuna Maafisa Ugani wa kutosha kupita kwa wakulima vijijini hasa katika Wilaya ya Iringa, Jimbo la Kalenga, Kilolo na Isimani. Nashauri Waziri anapojibu hoja hizi atueleze ni lini wananchi wa Wilaya ya Iringa watapatiwa Maafisa Ugani wa kutosha?
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri mkulima awezeshwe bajeti ya mbegu, mbolea na viatilifu (pesticides). Wakulima ambao wanatumia madawa hayo kwenye mazao mara nyingi magonjwa hayaishi mfano ugonjwa wa kantangaze kwa sababu madawa haya wakati mwingine ni feki. Makampuni mengi yanauza madawa yasiyofaa, Waziri afuatilie na kuzingatia hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mbolea zinazotumika ni za gharama kubwa mfano yara. Mbolea hii mfuko mmoja ni Sh. 90,000 wananchi wa kawaida hawawezi kumudu kutumia na hivyo kusababisha kuzalisha mazao yasiyo na ubora.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha umwagiliaji ni suluhu kwa uzalishaji mazao mbalimbali. Wizara ihamasishe kilimo cha matone lakini wakulima wawezeshwe kwani hawataweza kumudu drip lines. Serikali itoe mitaji kwa wakulima na pia iwe na Benki ya Wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Kiwanda cha Chai kilichopo Wilaya ya Kilolo, mpaka leo hii kimefungwa na kinakatisha tamaa wakulima wa chai wa wilaya hiyo. Naomba Serikali itoe majibu ni lini kiwanda hiki kitaanza kuzalisha ili wakulima wa chai waweze kujikwamua kiuchumi?