Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na timu yote ya Wizara kwa utekelezaji wa majukumu yao ya Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya sababu ya kutofanya vizuri kwa vijana wetu katika mitihani ya kidato cha nne na sita ni lugha ya kiingereza. Lugha hii ndiyo inatumika katika kufundishia vijana wengi lakini hawaelewi kiingereza. Napendekeza kwamba vijana baada ya kumaliza darasa la saba kabla ya kuanza masomo ya sekondari watumie mwaka mmoja wa matayarisho na kuwaweka katika kukielewa kiingereza, yaani tuwe na utaratibu wa pre- form one kwa mwaka kwa kuwawezesha katika kukielewa kiingereza na hisabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Malinyi tunaomba Mheshimiwa Waziri kupitia TEA juu ya ukamilishaji wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari ya Kipingo Malinyi. Ombi lilikubaliwa lakini hadi leo hakuna utekelezaji. Tunamwomba Mheshimiwa Waziri atupatie kipaumbele, ombi la Malinyi Wilaya ambayo haina kabisa shule ya sekondari ya bweni wala hakuna high school kwa Wilaya yote ya Malinyi. Ahsante.