Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna kata 15 na kuna shule za sekondari za kata nane tu ambazo zote ni za kidato cha kwanza mpaka kidato cha nne. Ninaomba angalau shule ya kidato cha tano na sita, moja au mbili ili kuwachukua wanaomaliza katika shule hizo. Kwani wengi wanaomaliza kidato cha nne wanabaki vijijini bila kuendelea mbele kidato cha tano wala vyuo. Hivyo kukatisha tamaa wanafunzi na wazazi wao kuonekana kuwa watoto walimaliza kidato cha nne wanaishia kuishi kijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna upungufu mkubwa wa madarasa, nyumba za walimu, maabara, mabweni na miundombinu ya library. Shule zote nane hazina library, hazina mabwalo ya chakula wala majiko ya kupikia chakula. Kutokana na tabia ya wananchi wa kusini, tunalazimika watoto wakae mashuleni kwenye shule zote za kata ili kupunguza utoro na kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Mhesimiwa Mwenyekiti, ipo idadi kubwa ya wanafunzi wanaopelekwa mashuleni kuliko miundombinu iliyopo. Mwaka 2016 na 2017 baada ya Sera ya Elimu bila malipo, watoto wengi wamekuwa wanafaulu kupelekwa kidato cha kwanza bila kuangalia miundombinu iliyopo katika shule hizo.

Hivyo Serikali iangalie namna ya kuwapeleka mashuleni kulingana na miundombinu ya mabweni, madawati, madarasa hata vyoo katika shule hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni upungufu mkubwa wa walimu wa sayansi. Shule zote zilizopo kwenye Jimbo langu, kuna upungufu mkubwa wa walimu wa sayansi, hivyo kufanya watoto wachukue masomo ya sayansi na wote kusoma masomo ya arts.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tunaomba Serikali kuajiri walimu wengi wa sayansi hasa hesabu, physics, chemistry na biology. Somo la kilimo (agriculture) lipewe kipaumbele kwa sababu ajira hamna, vyuo ni vichache, havitoshi ili watu tu wajifunze kilimo chenye tija zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu, kuna Shule za Msingi ambazo mpaka leo zimeezekwa kwa nyasi pamoja na nyumba za Walimu. Ninaomba Serikali ione namna ya kuzisaidia shule hizo ambazo ni Mbati ya leo Mkambala, Mchangani, Mrusha, Tupendane, Tukaewote na Mchangamoto.