Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa na mimi fursa ya kuweza kuchangia Wizara hii ya Maji. Na mimi pia niungane na wenzangu kusema kwamba maji ni uhai, maji ni uchumi wa viwanda na hasa kilimo pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ninachosikitika ni kwamba ndugu zetu wanasifia, wanasifia halafu wanadai, wanalia. Mimi napenda kuwaeleza Mheshimiwa Waziri kazi yako unaifahamu kama Wizara, jukumu lako ni kutafuta fedha, kuandaa miongozo ya utekelezaji na kutoa ushauri wa kitaalam. Mikoa kazi yao ni kusimamia na kutoa ushauri wa kiufundi na Halmashauri zetu kazi zake ni kutekeleza miradi ya maji vijijini. Kinachoshindikana kwetu ni wewe Waziri kushindwa kutekeleza wajibu wako. Umeshindwa kututafutia fedha, kwa nini umeshindwa kutafuta fedha? Kila Mbunge anakulilia kuhusu maji. Angalia bajeti yetu tuliyoipitisha ni kwamba tulipitisha shilingi bilioni 623.6 lakini ukashindwa kutafuta hizo fedha umetupatia shilingi bilioni 135, asilimia 22; ni wajibu wako. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ni wajibu wako kwa nini hukwenda kumlilia mwenzio, Waziri wa Fedha yupo hapa, mko naye kila kila siku, mpo nao kwenye Baraza lenu la Mawaziri mmeshindwa kututafutia hizo fedha, kuna nini au kuna mtu mwingine ameshikilia hii hela kwa sababu wapitishaji na waidhinishaji ni Bunge na Bunge likipitisha maana yake ni fedha na kodi za wananchi, siyo hela ya mtu binafsi. Kwa nini hizi hela zimeshindikana kuja kwenye mradi wa maji, kosa lipo kwako, tutakulaumu. Watu wanasema wewe ni mgeni, wewe sio mgeni kwenye Baraza hili la Mawaziri, ulikuwa Naibu Waziri wa Maji, kwa hiyo, wewe sio mgeni na Wizara, hakuna ugeni kwenye Wizara, wewe sio mgeni unafahamu kila kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo muhimu ya kuzungumza ni kwamba, je, maji ndiyo kipaumbele au bombardier ndiyo kipaumbele au standard gauge ndiyo kipaumbele. Waziri alipokuwa anatoa hotuba hapa, glass ya maji iko karibu yake, ya nini? Maana yake anataka kutengeneza uhai wake. Mlipokuwa kwenye Tulia Marathon nimewaona kabisa mmebeba maji, ya nini kama sio muhimu? Mimi nadhani maji ni muhimu na tuangalie suala la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi napenda kuzungumzia suala la fedha zilivyotafutwa ambapo ameshindwa Waziri na tunakulaumu wewe Waziri kwa kweli kushindwa kutafuta hizi fedha. Kulikuwa na BRN ya kutekeleza miradi ya vijijini na hiyo BRN ilienda wapi? Zile shilingi trilioni 1.45 zipo wapi, za miaka mitatu iliyopita? Ina maana kwamba fedha zile zilipatikana, zilipokwenda vijijini hazikufanya kazi halafu wewe ukienda vijijini kule kutembelea miradi unapokelewa na Mkuu wa Mkoa/Mkuu wa Wilaya unaenda kupelekwa kwenye mradi mmoja tu kumbe miradi mingine yote ni mibovu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Kamati ya LAAC, CAG anatuelekeza kabisa kusema kwamba miradi ni mibovu na kweli tukienda kukagua miradi yote ni mibovu haijatekelezeka halafu kwenye kitabu chako huku umeandika miradi yote imetekelezeka, haikutekelezeka. Ndiyo maana tunaomba kuunda Tume ambayo itaenda kuangalia haya masuala na ni watumishi wako wanaofanya hiyo kazi na wewe hukwenda kuwasimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna miradi ya Same – Korogwe ambayo imetolewa taarifa yake. Tangu mwaka 2014 ilitolewa fedha dola milioni 41.36, ni kutengeneza mradi huo ambao mmeuweka tena mwaka huu, sijui wa kuweka dawa, kutandika bomba, sijui wa kitu gani, haukutekelezeka.