Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuipitisha familia yangu katika kipindi hiki kigumu ambacho mdogo wetu Suguta alichomwa kisu na polisi kwenye Kituo cha Polisi akiwa amefungwa pingu na akafariki dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo moja linalonisikitisha, sijui ni kwa makusudi au ni kwa bahati mbaya, haijatoka official statement ya Serikali kwa maana ya Waziri anayehusika kukemea au kulaani kitendo kile kiovu kilichofanywa na polisi. Kwa hiyo, hilo namuachia Mungu na kwa sababu wao wanafikiri wako salama waache wajidanganye.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii inashauriwa mara nyingi na mimi nasikitika mipango ya Serikali ya CCM ni mipango ya miaka miwili au mwaka mmoja na ndiyo maana mipango mingi ina-fail. Mngekuwa mnachukua mawazo hapa na mnayafanyia kazi mmengekuwa hampati matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama mnakumbuka wakati mnajenga kituo cha DART pale, Mheshimiwa Mnyika aliwaambia kwamba hapa huwa panajaa maji na wakati ule Rais huyu wa sasa akiwa Waziri. Mmejenga pale kituo kwa mabilioni ya pesa za Watanzania, leo kinajaa maji. Hiyo ndiyo mipango yenu, miaka miwili haijapita kituo kinajaa maji pale mafuriko. Sasa nimeona gazeti la leo linasema mnataka mhamishe kituo pale mpeleke Ubungo, pesa mlishawekeza pale, nani analipa hizo pesa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili suala la maji na tuelewane vizuri, Mheshimiwa Kamwelwe wewe umeenda Tarime ukakimbia hukutuambia sisi, ukaenda. Kuna miradi pale Waziri Mkuu amekuja ameiona, mradi kwa mfano wa Gibaso shilingi milioni 900 imepelekwa hautoi hata tone la maji. Leo watu wanasema hapa tuunde Tume ya Kibunge ipitie miradi nchi nzima ilete taarifa Bungeni siyo kwa ajili yako, kuangalia hawa watu waliopelekewa pesa na wamekula pesa za walipa kodi wengine wanasimama hapa wanapinga, sasa mnapinga nini yaani hata hamueleweki.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu miradi imepelekewa pesa, pesa zimeliwa leo mnakuja hapa Wabunge mnasema muweke tozo shilingi 50 kwa wananchi maskini ambao mmeweka kwenye REA, pesa za REA mmeweka shilingi 50 haziendi mpaka sasa, miradi ya densification na miradi ya REA imesimama. Pesa hizi muweke kwa mama anayesaga kwa mafuta ya dizeli, mama ambaye anapanda bodaboda kijijini, mama ambaye ananunua mafuta ya taa mumuwekee ongezeko la shilingi 50, mumuumize wakati tunajua na tuna uhakika hamtapeleka maji wala hayo maji hayatapatikana. Sasa hii kitu haikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana tunasema Engineer Kamwelwe uliambie Bunge hili, mwaka jana ulituambia kuna dola milioni 500 kutoka Serikali ya India, zipo wapi hizo pesa? Kama umesahau sisi wengine tuna kumbukumbu, tunakukumbusha, zipo dola milioni 500 ambazo mlituambia kwamba zipo kwa ajili ya maji vijijini, zipo wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo nimesoma kitabu hiki cha kwenu, mama Makilagi amesimama pale anachangia Mbunge aliyepita sasa hivi amezungumza hata kwa Mwalimu Nyerere hakuna maji. Mimi nimezaliwa Tarime maji yapo, miaka ya 1980 watu wanatumia maji ya bomba. Kadri tunavyoenda mbele tunarudi nyuma yaani leo mwaka 2018 hakuna maji ya bomba, mwaka 1980, 1985, 1986 kuna maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sisi tukiwaambia bora wakoloni kuliko ninyi Serikali ya CCM hivi mnapinga nini? Kama wakoloni waliacha mabomba, leo hata mabomba waliyoacha yamekufa, yamewashinda, hivi ninyi mnapinga nini sasa hapo yaani mnapingana na nini kwa sababu Serikali yenu imeshindwa.