Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru sana Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa jitihada kubwa anazofanya katika kutuletea maendeleo katika nchi yetu. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Maji kwa jitihada kubwa anazofanya katika sekta hii ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kwa kweli kumshukuru kwa dhati, kulikuwa na tatizo la muda mrefu la fidia ya watu wa Selembala katika Jimbo langu, fidia ambayo zaidi ya miaka minne tumekuwa tunahangaika nayo lakini kwake yeye amelifanikisha na wananchi wamelipwa jumla ya shilingi bilioni 3.3. Siyo pesa ndogo, amejitahidi namshukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo changamoto ndogo ndogo ambazo bado sekta hii tunaiomba itusaidie kupitia kwa Waziri. Moja, yapo maeneo katika Jimbo la Morogoro Kusini ambayo kwa kweli yanapewa maji ya visima, lakini hayastahili kunywa maji ya visima. Zipo sehemu za Sesenga na maeneo ya Kisaki, nashauri tuwe na mradi wa kupeleka maji ya bomba. Hili linawezekana kwa sababu tuna mito mikubwa tu ambayo ipo maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nitaliomba kwa Mheshimiwa Waziri ni kuangalia uwezekano wa kuwa na mradi ndani ya Jimbo lile wa kueneza mabomba ya maji, yachukue kutoka kwenye vyanzo vya mito ili wananchi wapate maji safi na ya uhakika, tuachane na visima. Yapo maeneo kweli yanastahili visima lakini sio katika jimbo lile ambalo limezungukwa na mito mikubwa, sehemu nyingi hizo na details zake nitampatia Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu nitakaloomba kwa Waziri, atakapokuwa anangalia uwezekano wa kutengeneza miradi mikubwa ya namna hiyo, aone wataalam waliopo katika halmashauri zake. Halmashauri zetu wakati mwingine tunakosa kuwa na miradi mizuri kwa sababu ya kukosa watu wenye uwezo wa kubuni na hili ni suala la utaalam. Nitamuomba sana aliangalie kwa upande wa Morogoro Vijijini ili tuweze kuwa na wataalam wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, langu mimi kubwa ilikuwa nimshukuru Waziri amefanya jitihada kubwa sana, ahsante sana.