Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja ya Wizara ya Kilimo katika mambo yafuatayo kwa ajili ya Mkoa wangu wa Njombe. Katika Mkoa wa Njombe kumetokea janga la viazi kuungua kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa. Hivyo wananchi wamepoteza mtaji katika zao hilo la viazi na kusababisha wakulima hao kukata tamaa kulima zao hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na wananchi hao kupata hasara kubwa na kupoteza fedha ambazo wengi wao walikuwa wamekopa na wanadaiwa na taasisi mbalimbali ambazo walikopa, naiomba Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuona namna ya kuwasaidia wakulima hao kuwatafutia mbegu kutoka nchi ya Kenya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ushuru wa mbao utolewe mara moja na siyo mara mbili au tatu kama ilivyo sasa. Ushuru hutozwa mbao zinapotoka porini, hutozwa mbao zinapoingia na kutoka kwenye maeneo ya halmashauri ambapo mbao zinaanikwa. Ushuru hutozwa tena zinapopita katika mageti ya barabarani zinaposafiri kwenda mikoa mingine kutoka Mkoa wa Njombe. Hivyo, naomba ushuru huo utolewe mara moja na kisha wafanyabiashara hawa wapewe risiti ambayo itaonyeshwa kwenye kila geti watakapopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mkoa wa Njombe ni kati ya mikoa mitano inayozalisha mazao ya chakula kwa wingi na kwa kuwa pembejeo ni gharama, naomba bei ya pembejeo ishuke kusudi wakulima wa Mkoa wa Njombe waweze kupata unafuu wa pembejeo hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.