Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumushukuru Mheshimiwa Waziri kwa kufanikisha malipo ya wapiga kura wangu walio katika Chanzo cha Maji Champala, kwa kweli nakushukuru kwa hili, Mwenyezi Mungu akujalie afya, busara na hekima.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kumshukuru Mheshimiwa Waziri naomba sana tatizo la maji katika Mji Mdogo wa Kilwa Kivinje ambapo ipo Hospitali ya Wilaya ambayo ina upungufu wa maji kwa muda mrefu. Nakuomba sana Mji Mdogo wa Kivinje uangaliwe kwa jicho la huruma sana, tena sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, napenda kukukumbusha Mradi wa Maji wa Mavuji ambao upembuzi yakinifu umekamilika lakini tatizo ni upatikanaji wa fedha kwa ajili ya mradi huo. Mradi wa Mavuji utakapopata fedha na kukamilika hilo ndilo suluhisho la upatikanaji wa maji katika Mji Mdogo wa Kivinje/Masoko. Nakuomba sana usimamie mradi huu wa Mavuji ambao upembuzi yakinifu ulifanywa na Wabelgiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naomba fedha zilizopangwa mwaka 2017/2018 zitolewe katika miradi ya maji na pia fedha zilizolengwa katika bajeti ya mwaka 2018/2019 zipatikane ili matatizo ya maji yapungue. Natanguliza shukrani, ahsante. Tunakuelewa na tunakukubali.