Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe pongezi za dhati kwa Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara hii na watendaji wote. Jambo kubwa la pongezi ni namna ambayo tayari juhudi kubwa za makusudi ambazo zimeanza kuonekana katika suala zima la kutatua tatizo la maji kwa wananchi wa Tanzania. Tumeona miradi mikubwa ikianzishwa. Hata hivyo nina ushauri kwamba hebu Serikali ichukue hatua za makusudi za kuunda tume maalum itakayochanganyika na Wabunge ili waende kwenye maeneo yote ambayo yalidumu kwa muda mrefu bila kukamilika ilhali Serikali inakuwa imetoa fedha za miradi hiyo ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni miaka zaidi ya kumi sasa niko ndani ya Bunge na kila mwaka nimeshuhudia tukipitisha bajeti ya maji hata kama ni kidogo. Je, fedha hizo ni kweli hadi sasa bado hazijatatua angalau kwa asilimia ndogo ya tatizo la maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, kweli inasikitisha kwani zaidi ya fedha za Serikali pia kuna fedha za wahisani zimekuwa zikiletwa nchini. Mimi nina mashaka huenda kuna chungio linapitisha fedha hizi. Hivyo nashauri tume iundwe na iangalie kuanzia miaka kumi iliyopita na fedha ambazo zimeshatoka na kama zilitumika ipasavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ni kwa nini Mkoa wa Singida hauna mradi mkubwa wa maji? Naomba na sisi Singida tupate mradi mkubwa wa maji utakaotatua tatizo la maji kwenye mkoa wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.