Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naunga hoja mkono na ninakupongeza Waziri, Mheshimiwa Engineer Kamwelwe, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, na timu yote ya Wizarani kwa kazi nzuri ya kuwapatia wananchi wa Tanzania maji safi na salama. Changamoto ni kuwa Tanzania imezungukwa na maziwa (lakes) kadhaa, lakini hatujaweza kunufaika nayo. Nini kifanyike ili vyanzo hivyo vya maji vinufaishe wengi?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uvunaji wa maji ya mvua, msimu wa mvua maji yanatiririka hovyo kila mahali na mvua zikiisha shida iko pale pale. Kwenye kitabu imesemwa kidogo sana, swali, ni lini sasa Serikali italeta Muswada hapa Bungeni wa kutunga sheria ya kuokoa kila tone la maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, haingii akilini kwamba Serikali inaingia gharama kubwa sana kutibu maji machafu hadi yawe safi na salama wakati ambapo yale ya mvua yaliyo safi naturaly yanapotea ardhini. Maji ya mvua yanayotiririka barabarani na kuharibu miundombinu yajengewe mabwawa. Mfano, maji yanayotiririka Kibaigwa, njia ya Dodoma – Dar es Salaam ni lini sasa maji hayo yatakingwa kama ilivyo Morogoro (Mindu Dam)?

Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza sana mamlaka zote za maji nchini, ombi, Wizara izisaidie kudai madeni ili zifanikiwe kuendesha shughuli zake kwa amani na utulivu. Taasisi za Serikali zinadaiwa hela nyingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi mabovu ya maji safi na salama viwandani, shambani/bustani, car wash na kwingineko; ombi, Serikali itujulishe mkakati wake wa kukomesha jambo hilo kwani maji safi na salama ni ghali sana; vifaa/taps za maji zinamwaga maji hovyo, Serikali itoe tamko kuhusu jambo hili. Kwenye taasisi, mashuleni na majumbani zitumike zile bomba za kuhisi (sensor).

Mheshimiwa Naibu Spika, usimamizi wa uchimbaji visima vijijini unaposimamiwa na wataalam Wizarani si mzuri kwani gharama zinakuwa mara mbili. Wengi wanaona ni vyema Halmashauri zikasimamia. Wizara isiingilie maji yanayosimamiwa na wafadhili, mfano Hai - Himo – Njia Panda; mradi unaosimamiwa na Kilema Kusini Water Users Association uwe huru kujiendesha kama ulivyo Mradi wa Uroki. Nashukuru kwa Mradi wa Mwanga/Same – Korogwe kutengewa hela. Naomba kuwasilisha.