Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia katika bajeti hii ya Maji na Umwagiliaji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, akinamama na watoto ndiyo wanaoumia zaidi na tatizo la kukosekana maji nchini Tanzania. Kama inavyojulikana akinamama ndiyo wapishi katika familia zetu za Kiafrika pamoja na watoto kwa maana ya kuwafundisha kazi kwa ajili ya maisha ya baadae. Mfano, katika Jimbo la Ngorongoro Kijiji cha Naiyobi, Mkoani Arusha kuna kero kubwa sana ya ukosefu wa maji kwa muda mrefu sasa, akinamama na watoto wanakesha hadi siku tatu kwenye bomba la kijiji kwa ajili ya kusubiria maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana tatizo la maji lishughulikiwe na kupewa kipaumbele kwa ajili ya kuwasaidia akinamama hawa ambao wamekuwa wanateseka na tatizo la maji kwa muda wa miaka 20 sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Ngorongoro ni Jimbo la kitalii kupitia Crater ya Ngorongoro ambayo pia ni kati ya maajabu ya dunia. Kama inavyojulikana sekta ya utalii ni sekta inayoongoza kuliingizia Taifa letu fedha za kitalii na pia kuongoza kwa kuongeza pato la Taifa baada ya madini ya dhahabu kushuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza Wilaya hii ipate ufumbuzi wa tatizo hili la maji ambalo limedumu kwa muda wa miaka 20 sasa.