Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, natanguliza kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri, pia pongezi kwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji kwa utekelezaji mzuri wa Ilani.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Bagamoyo wanaishukuru Serikali kwa kujengewa tenki kubwa la maji Mjini Bagamoyo, huu ni ukombozi wa huduma bora za maji safi na salama kwa wananchi wa Mji wa Bagamoyo na maeneo ya jirani. Kwa vile tenki sasa limekaribia kukamilika je, mradi wa usambazaji wa mabomba lini utaanza? Pia mradi wa usambazaji mabomba ya maji utahusu kata zipi za Jimbo la Bagamoyo? Tunaomba Mheshimiwa Waziri atupe majibu ya maswali haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa CHALIWASA unahudumia vijiji vya Mwavi, Fukayosi na Makurunge katika Jimbo la Bagamoyo ila huduma ya maji kwa vijiji hivi imekuwa hairidhishi tangu mradi umeanza. Mabomba ya CHALIWASA hayatoi maji. Napendekeza Wizara ibuni mradi wa maji kutoka Mto Ruvu katika eneo la Mtoni ili kuhudumia vijiji vya Kata za Makurunge na Fukayosi kwa upande wa Jimbo la Bagamoyo. Huduma ya maji katika kata hizi ni duni sana. Mheshimiwa Waziri atujulishe mpango wa Serikali juu ya kuwapatia maji wananchi wa Makurunge na Fukayosi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.