Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, vyanzo vya maji katika nchi hii vinahitaji kuhifadhiwa kwa nguvu kubwa kwani kasi ya kuharibiwa ni kubwa mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa alipofanya ziara Bonde la Eyasi mwaka 2016 alitoa kauli za Serikali zifuatazo:-

(a) Chanzo cha Qangded kihifadhiwe kwa radius ya mita 500 pande zote.

(b) Mashine zote zilizoko mtoni ku-pump maji ziondolewe na ziwekwe nje kabisa ya chanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi leo miezi 17 tangu tamko litoke hakuna lililofanyika. Nimuombe Waziri wa Maji na Umwagiliaji afike Bonde la Eyasi ili kutekeleza maagizo hayo ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Kijiji cha Getamvua uliojengwa chini ya WSPP kwa zaidi ya shilingi milioni 600 haufanyi kazi kwa kujengwa chini ya kiwango. Wataalam wa Wizara walienda kufanya tathmini na hadi leo fedha za ukarabati bado hazijaletwa. Nimuombe Waziri awakumbuke wananchi wa Getamoa ili mradi ule wa maji ufufuliwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Karatu kwa kushirikiana na Shirika la Kidini la CRS wamefanya mradi wa maji katika kijiji cha Qaru kwa kutumia mfumo wa prepaid water meters. Mfumo huo una mafanikio makubwa sana kwani hata mapato yameongezeka mara tatu. Tunamuomba Waziri afike azindue mradi huo ili kutoa hamasa kwa wadau wengine.