Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya bajeti ya Wizara hii. Aidha, nimpongeze Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya maji, baadhi ya watendaji walioko kwenye Halmashauri hawasimamii ipasavyo. Kumekuwepo na ubadhirifu ambao umepelekea kujengwa miradi iliyo chini ya viwango. Ninao mfano wa Halmashauri ya Igunga, mradi ulikamilika lakini wananchi hawapati maji na tenki kubwa likijazwa maji linavuja. Kamati ya LAAC imeagiza CAG akague mradi huo. Aidha, miradi mingi iliyotekelezwa ya World Bank haipo sawa, ni vema Mkaguzi Mkuu (CAG) akaikagua miradi hii ili tuweze kujua zaidi hali halisi kwani fedha hiyo ni ya jasho la wananchi ambao watarejesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Korogwe Mjini tumeanzishiwa mradi wa maji kwa kupewa shilingi milioni 500. Mradi huu tenki limekamilika tatizo ni miundombinu ya kusambaza maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna mradi ulitengewa fedha wa vijiji kumi vya Lwengera Darajani, Relini na Msambiazi. Nashukuru Msambiazi mradi upo karibu kukamilika asilimia 80 mpaka 85, tenki limejengwa na virura vimeshajengwa, mkandarasi hajalipwa na ndiye aliyepewa mradi wa Lwengera Darajani/Relini. Naomba Wizara imlipe mkandarasi huyu kwani madai yake (certificate) zilishawasilishwa ili aweze kuendelea na kazi ya Lwengera Darajani, vinginevyo Wizara inafanya kazi vizuri anahitaji kupewa fedha ili kukamilisha miradi iliyopo.