Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naunga mkono hoja hii na nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na viongozi wote wa Wizara hii kwa namna wanavyojituma katika kutatua tatizo la maji nchini. Naomba yafuatayo yazingatiwe:-

(i) Uendelevu wa huduma ya kutoa maji lazima baadhi ya mifumo ya uendeshaji ifanyiwe utafiti.

(ii) Programu ya Maji (WSDP) inawatekelezaji wengi ambao wanatofautiana sana katika approach ya utendaji. Wizara imetengeneza sera lakini watekelezaji wake hawako chini ya Wizara kwa mfano Halmashauri za Wilaya na kadhalika. Nashauri katika suala la utekelezaji au ufungaji wa miradi wa maji vijijini na usimamiwe na Wizara.

(iii) Tuongeze juhudi za uvunaji wa maji ya mvua, tujenge mabwawa mengi ili kuongeza rasilimali za maji na hili lisimamiwe na Wizara. Katika hili Jimbo langu la Wanging’ombe katika bajeti 2017/2018 Wizara ilipanga kufanya upembuzi na usanifu wa kujenga Bwawa la Ulembwe na Igwadianya, nataka kujua hatua ya utekelezaji na naomba mabwawa hayo yajengwe.

(iv) Mradi wa Mbukwa ulijengwa na UNICEF miaka ya 1976 ni chakavu ijapokuwa inahudumia zaidi ya vijiji 50. Najua toka Awamu ya Nne Serikali iliahidiwa na Serikali ya India kuwa mradi huu utaboreshwa. Nimeona kwenye hotuba zimelengwa dola za kimarekani milioni 48.99 kwa ajili ya kukarabati mradi huu. Naomba kwanza kuishukuru Serikali kwa kufuatilia utekelezaji wa mradi ili wananchi hasa wa kata za Wanging’ombe, Saja, Kijumbe, Ludinga, Ilembula na Uhamhule wanashida sana ya maji na hasa kuanzia mwezi wa sita (wakati wa kiangazi).

(v) Mheshimiwa Waziri ulitembelea Jimbo langu na uliahidi visima viwili katika Kijiji cha Ihanjulwa na Itulahimba, wananchi wale walikuchezea ngoma kwa imani kuwa utawaondolea kero ya maji.