Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono na kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Maji na Naibu Waziri na wasaidizi wake wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa miradi mikubwa inayotekelezwa jimboni kwangu. Nina mradi mkubwa wa kijiji cha Majalila na kijiji cha Igagala imetekelezwa na kutoa huduma kubwa sana kwa wananchi.

Naiomba Serikali kupitia Wizara juu ya miradi ya Mwese, Ilangu, Kamjela na Kabungu ambayo bado haijatekelezwa. Tunaomba Wizara isimamie kutekelezwa kwa miradi hiyo ambayo itawasaidia wananchi katika vijiji hivyo nilivyovitaja na ilitengewa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba ukarabati ufanyike katika visima katika vijiji vya Mishamo ambavyo vilichimbwa na Shirika la Wakimbizi la UNHCR mwaka 1978. Tunaomba vikarabatiwe ili viweze kutoa huduma ya maji kwenye vijij hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa ukarabati wa vijiji hivyo vya Ilangu, Bulamata, Kamjela, Ifumbula, Mazwe, Kapemba, Isenga Mazwe, Kusi Rugufu, Kabanga, Mgansa, Busongolala, Ipwaga na Mlibansi kunaweza kutatua tatizo la maji kwa gharama nafuu. Naomba sana vijiji hivi mvipatie fedha za kukarabati visima.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Kijiji cha Ngomalusambo uliibiwa fedha, tunaomba wahusika wa mradi huu wachukuliwe hatua kwani mradi huu umesababisha hasara zaidi ya shilingi 280,000,000 ambazo zimetumika bila kutoa maji. Wahusika wapo na hakuna hatua iliyochukuliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo la ukosefu wa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo ya maji. Hivyo tunaomba Serikali iongeze tengo la fedha ili tuweze kutekeleza miradi na mahitaji ni makubwa sana kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali katika utekelezaji wa miradi iwe na udhibiti mkubwa ili iwe na tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.