Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Maji Kasamwa ni tegemeo kubwa kwa wananchi wa Kasamwa kwa kuwa visima vyote huwa vinakauka wakati wa kiangazi. Hivi sasa Bwawa la Kasamwa limepasuka kutokana na mvua kubwa. Naomba Wizara
ifanye ukarabati mkubwa katika bwawa hili ambalo hivi sasa limepasuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hali ya maji Kasamwa, Mji wa Kasamwa una watu wanaokadiriwa kuwa 25,000 ambao wanategemea visima. Naiomba Serikali kupeleka maji ya bomba kutoka Geita Mjini kwa kuwa umbali uliopo kutoka Geita Buhalahala kwenda Kasamwa ni kama kilometa 10 umbali ambao ni mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya maji Ihanamilo, Nyanguku, Mgusu na Bulela. Hizi ni kata ambazo ni sehemu ya Geita Mjini lakini hazimo katika hotuba ya Waziri na hali ya maji katika kata hizi ni mbaya sana. Naomba Serikali badala ya kufikiria kuchimba visima ni vyema kuweka mkakati wa kupeleka maji ya ziwa ya bomba ambayo yapo ndani ya kilometa 30 tu kutoka makao makuu ya mji.