Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa shukrani zangu kwako kwa kunipa fursa hii ya kutoa mchango wangu katika hotuba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji. Aidha, nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa uongozi wao wa kuongoza Wizara hii nyeti katika nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuchangia Wizara hii, naomba kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Wizara kwa kuendelea kujenga na kuimarisha vyanzo vya maji nchini, mijini na vijijini na pia kuimarishwa Mamlaka za Maji katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu katika suala la vyanzo vya maji ni kusimamia na kuchukua hadhari kubwa ya namna ya kuyatunza maji. Siyo sahihi kuona kwamba mahodhi ambayo yanahifadhi maji huwekwa wazi bila ya kufunikwa. Anaweza kutokeza adui akarusha kitu cha kudhuru (sumu) kwenye maji na akasababisha madhara makubwa kwa wananchi. Mfano wa suala hili ni katika Mamlaka ya Maji Mwanza (MWAUWASA). Katika Mamlaka hii hodhi la kuhifadhia maji liko wazi. Kwa hiyo, naiomba Wizara ielekeze mamlaka husika ichukue hadhari/udhibiti wa suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.