Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Mto Mgembezi unalenga kutoa maji kwenye vijiji zaidi ya 15 toka chanzo chenye uhakika cha mto huu. Mradi huu ulishafanyiwa upembuzi yakinifu miaka ya nyuma na kuonekana gharama yake ni shilingi bilioni 10. Hata hivyo, mradi huu umeshajengwa intake ya zaidi ya shilingi milioni
200. Hivyo bado kazi ya kutandika mabomba na ujenzi wa tanki la kuhifadhi maji. Mradi huu unaweza kufanyika kwa awamu mbili kama ifuatavyo:-

Awamu ya kwanza ni kutandika bomba hadi Kakonko Mjini na kujenga tenki kubwa kwa kuyasambaza Mjini Kakonko na awamu ya pili ni kuyasambaza kwa vijiji vya jirani vya Kata za Kanga, Kakonko, Kiziguzigu na Kasanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji ya BTC waliahidi kuweka miradi ya maji katika vijiji vya Wilaya ya Kakonko. Vijiji hivyo ni Kakonko, Mbizi, Itumbiko, Muganza, Kiziguzigu, Ruyewizi na Kabingo. Miradi hii imekwama hadi sasa haijaanza kutekelezwa. Serikali ieleze ni lini miradi hii itaanza kutekelezwa ili wananchi waliopewa matumaini waanze kunufaika?

Mheshimiwa Naibu Spika, ipo miradi mitano katika Wilaya ya Kakonko ambayo imekamilika lakini haitoi maji wakati miradi ilishakabidhiwa na kulipwa fedha zote hata za retention. Miradi hiyo ni Nyagwijima, Kiduduye, Katanga, Muhange na Kiga (huu una nafuu). Miradi hii ilifanyiwa ufisadi wa hali ya juu na hivyo hakuna value for money.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri kwamba waliohusika na ubadhirifu wachukuliwe hatua yaani wakandarasi na wasimamizi wa miradi hiyo, yaani wahandisi wa Kibondo na Kakonko, maana ilianza kabla ya kugawa Wilaya za Kakonko na Kibondo. Naomba miradi hii ifanyiwe tathmini ili kujua inahitaji nini ili iweze kuhudumia wananchi baada ya kufanyiwa marekebisho muhimu yanayohitajika.

Mheshimiwa Naibu Spika, vipo visima Wilaya ya Kakonko katika vijiji mbalimbali ambavyo vina maji lakini vina miundombinu mibovu ya visima kama vile pump, rubber na kadhalika. Visima hivi vinashindikana kutengenezwa kwa nguvu za wananchi kutokana na gharama za vipuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri zianzishwe Kamati za Maji za Vijiji vyote vyenye visima ili Kamati zikusanye fedha kwa watumiaji wa maji zitakazotumika kukarabati miundombinu ya visima. Pia nashauri Idara ya Maji, Wilaya ipewe uwezo kifedha ili wataalam wake wawe wanakagua visima hivyo mara kwa mara kwa kuvifanyia service.

Mheshimiwa Naibu Spika, Miradi ya Umwajiliaji ndio pekee inayoweza kulitoa Taifa hili katika uhaba wa chakula pindi ukame unapoathiri nchi hii na pia msimu wote wa mwaka yaani kiangazi na masika. Hivyo nashauri iwepo miradi mikubwa ya kitaifa kwa kanda. Kila kanda iwe na Irrigation Scheme kubwa ya mazao yanayostawi kanda hiyo. Pia kila Wilaya iwe na Irrigation Schemes zenye uwezo wa kilimo cha mwaka mzima yaani kiangazi na masika (sustainable irrigation schemes).