Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia juu ya udhibiti wa vifaa vya usambazaji wa maji (water supply accessories) na madawa ya kutibu maji (water treatment). Inabidi tujiulize, ni nani anadhibiti ubora na bei ya vifaa hivi na madawa ya kutibu maji? Je, Wizara inajua kinachoendelea? Je, kuna chombo chochote kinachoshughulikia hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, uharibifu wa miundomibinu huchangiwa na kukosekana kwa taarifa sahihi za ubora. Kwa kuwa soko ni huria na wakandarasi wanatafuta faida, hivyo ni wazi watakimbilia cheap price ili kupata faida kubwa at the end.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuhusu madawa ya kutibu maji, je, Wizara ina mechanism gani ya kujiridhisha kuwa mamlaka zote zinazosambaza maji nchini zinawajibika kutibu maji ili kutunza afya na uhai wa Watanzania?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni chombo gani ndani ya Wizara chenye jukumu la kuhakikisha udhibiti wa upatikanaji wa madawa ya kutibu, kusambaza na kupanga bei? Kuliacha soko liamue juu ya bei ya vifaa vya usambazaji maji na madawa ya kutibu maji bila udhibiti, kutaendelea kulitia hasara Taifa kwa kuwa na miundombinu isiyo na ubora.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kukosekana kwa uhakika kuhusu usalama wa Watanzania wote wanaotumia maji kwani hakuna uhakika kama nguvu ya soko inaweza kuratibu upatikanaji wa madawa yenye ubora na kwa bei sahihi ya soko. Hali hiyo pia husababisha kila mamlaka kujipangia bei yake ya huduma ili kufidia gharama zisizothibitika za madawa na vifaa. Kwa mfano, Wizara ya Afya inadhibiti usambazaji na bei kupitia MSD.