Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuchangia hoja iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ile kaulimbiu ya kumtua mwanamke ndoo bado haijatekelezwa kutokana na jitihada za Serikali zinazoonesha kwenda kidogo kidogo katika kuwapatia wananchi wengi maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga kuna baadhi ya vijiji bado havina maji, kuna mabomba lakini hayatoi maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata ya Madanga Wilaya ya Pangani kuna vitongoji ambavyo havina maji. Vitongoji hivyo ni Zimbiri, Jaira, Barabarani, Nunda na vinginevyo wananchi wanasaidiwa na maji ambayo taasisi za dini wamechimba visima.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ije na majibu ya lini Kata ya Madanga, Wilaya ya Pangani watapata maji safi na salama?

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika Kata ya Mwalijembe Wilaya ya Mkinga wananchi wana tatizo la maji, wanashirikiana maji yao na wanyama. Maji ya kwenye mabwawa siyo safi na salama. Serikali iwahurumie wananchi hawa ili kuwaepusha na magojwa ya mlipuko.