Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia asubuhi hii ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sio muumini wa ushirikina ingawa kuna wengi wanaamini katika ushirikina. Kila nikiangalia mazingira rafiki yenye kuvutia, yenye uwezo wa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda kuanzia ukubwa wa ardhi yenye uwezo wa kustawisha mimea ya kila aina, aina ya mifugo tuliyokuwa nayo, idadi ya watu, kwa maana ya soko la ndani, malighafi muhimu kwa maana ya chuma, makaa ya mawe na madini utayataja kadri utakavyoweza, uwepo wa bandari kubwa tatu zenye uwezo wa kufanya kazi katika standard za kimataifa na bandari nyingine ndogo ndogo kwenye maziwa na bahari isiyokuwa na idadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi imekaa vizuri kimkakati, inazungukwa na nchi nane ambazo zote zinatutegemea. Tuna mtandao mzuri wa barabara za lami ambao nchi za Afrika Mashariki na Kati hakuna nchi hata moja iliyounganishwa vizuri kwa mikoa na wilaya kama nchi yetu, na bado tuna reli na tunaendelea kutengeneza reli ya kisasa ya standard gauge. Kwa hizi sifa zote nzuri tusipokuwa na viwanda vya uhakika napata shida na ndiyo maana ninasema huenda tumerogwa. Kama huyo aliyeturoga sijui ni nani na kama kuna mganga wa kutugangua huko tulikorogwa basi atusaidie. Haiwezekani tukawa na nchi nzuri kama hii, yenye haya mambo mazuri yote leo hii tunasua sua kwenye viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi zote zilizokua kiviwanda dunia nzima zilianza na mahitaji ambayo wananchi wake wanayahitaji sana. Nchi ya Ujerumani ilipoanza viwanda ilianza na makaa ya mawe na chuma; nchi ya Uswisi ilipotaka kukua kwa viwanda ikaanzisha viwanda vidogo vidogo vya jibini, maziwa pamoja na mboga mboga; nchi ya Uholanzi ilipotaka kukua kwa viwanda ilianza kwenye maua na mboga mboga; nchi za China na India zilipotaka kukua kiviwanda zilijielekeza kwenye viwanda vya nguo. Kila nchi inakuwa na ajenda mahsusi inapotaka kwenda kwenye viwanda kulingana na mahitaji halisi ya watu wake, lakini vilevile kwa soko linalowazunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ina bahati ya kuwa na ajenda mahsusi ya viwanda. Tanzania ya viwanda ni national strategy ambayo wimbo huu ukipigwa unapaswa uchezwe na kila Mtanzania na katika tune ya ule muziki uliochezwa. Tunachokiona kwenye huu mkakati mkubwa wa kitaifa wa kuifanya Tanzania ya viwanda ni kana kwamba Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji inacheza muziki wake na wengine hao ambao inabidi waifanye hii Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji iende vizuri nao wanacheza muziki wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mwaka wa tatu sasa ta Tanzania ya viwanda. Sikilizeni bajeti zote hapa, tutaanza na Wizara ya Kilimo, wapi mtu wa kilimo ana-link mipango yake ya kilimo na viwanda tangu mwaka 2016 wapi ana- link, anakuja na mkakati wa kilimo unaoenda sambamba na Tanzania ya viwanda. Twende kwenye Wizara ya Mifugo na Uvuvi yote watakayosema na hotuba zao watakazozitoa wapi wana-conclude kwa kufanya moja, mbili, tatu kwenye kilimo, mifugo na uvuvi. Hapa sasa ndipo dirisha la kutokea kwenye viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, twende kwenye Ardhi. Mikakati ya mashamba, mikakati ya kurasimisha maji, wapi tuna-link ardhi na viwanda. Twende kwenye elimu, tutakwenda kutengeneza viwanda nchi nzima, mafundi michundo wako wapi? Wapi tume–link VETA na Tanzania ya viwanda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa haya yote hayawezi kwenda bila fedha. Ili twende kwenye Tanzania ya viwanda namba moja sasa mwezeshaji huyu fedha ndiye a-pump pesa kwenye haya maeneo manne niliyoyatoa ndipo hatimaye mtapata viwanda. Waziri wa Fedha asipoelekeza nguvu zake kwenye kilimo, asipoelekeza nguvu zake kwenye mifugo, asipoelekeza nguvu zake kwenye elimu hiyo Tanzania ya viwanda haiwezekani. Nilianza kwa kusema mwanzoni zile sifa nne/sita za Tanzania zina kila kitu kizuri, kwa nini hatuendi? Ndipo tunaishia kusema kwamba pengine tuanze kuamini na ushirikina, pengine tumerogwa na kama kuna mganga aje atugangue, sitaki kuamini hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchawi wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe na mganga wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe. Tunachohitaji sasa hivi ni kuthubutu kwa dhati, Watanzania wote tucheze tune moja, Watanzania wote tupate uelewa. Leo hii tunaongelea Tanzania ya viwanda, leo hii tunaangalia Tanzania ya viwanda yenye changamoto nyingi, lakini mahitaji yetu sisi hatukuwahi kujitosheleza kwa kila kitu. Tuanze tu na sembe, tunalima mahindi kule Kusini, tunalima Rukwa mahindi, mahindi yanafika yanatujalia hatuna uwezo hata wa kuyafanya yale mahindi angalau yasubiri misimu miwili kuangalia soko linakwendaje au tunasaga kwa kiasi gani kuwasaidia na majirani zetu. Kwa hiyo, tutakwenda kwa mwaka mmoja hatuna maghala, mahindi yataoza mwishowe tunaharibikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachotaka kukisema, sisi tuna changamoto nyingi lakini zote zinatibika. Tulivyotaka kutengeneza standard gauge hatukujadiliana na mtu tukaanza tu kwenda, hali kadhalika viwanda tunavyotaka kuweka. Tunapozungumzia Mchuchuma na Liganga hatuhitaji tena maneno kwa sababu tuna uhakika Tanzania ya viwanda inahitaji umeme wa kutosha, inahitaji chuma cha kutosha. Sasa Mchuchuma na Liganga tuna yote mawili kwa wakati mmoja. Una-caal hapo hapo na una-steel hapo hapo na ukienda kusoma kwenye historia za nchi zilizokuwa kwa viwanda unakuja kukuta Ujerumani walianzia hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii huu ukanda wetu huu tunaongelea ile story ya mafuta, sijui mchikichi, sijui alizeti, hivi tunashindwaje leo kuwaambia jamani JKT hebu kaeni, Magereza kaeni, wataalamu wa SUA hebu fanyeni breeding nzuri ya mbegu ya alizeti au mbegu ya mchikichi tuiweke ndani ya miaka mitatu/minne tusiwe na tatizo la mafuta au tunaongelea mambo ya sukari? Sitaki kuyasema haya, yamesemwa sana. Tanzania ya viwanda ianze na yale mahitaji. Tunakwenda kwenye nyama Tanzania yetu ni nchi ya pili kwa kuwa na ng’ombe wengi Afrika, lakini tujiulize maeneo yote ambayo wanahitaji nyama kwenye mahoteli nyama zinatoka wapi? Sasa hivi tunaongelea suala la maziwa, hatuna sehemu ya ku-process maziwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tutakwenda kwenye msimu wa nyanya, Waheshimiwa Wabunge, ninyi ni mashahidi mnapita hii njia mnafika pale Dumila, mnakuta nyanya zimemwagwa pale chini, nyanya zinauzwa mpaka shilingi 200 na hakuna mnunuaji. Hivi kweli tumeshindwa hata kuwasaidia kuwapa mawazo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kitu kimoja, Mheshimiwa Mwijage usidhani kwamba Watanzania unaposema viwanda wanaelewa kama unavyoelewa wewe. Wenzako wanaelewa kwamba wewe ndiye mwenye ajenda ya viwanda, wewe utawapelekea mashine na si kwamba wao wafikiri kulingana na mazingira yao. Hata hivyo ukitoa tafsiri ya viwanda, kama ulivyotuwekea, kwamba viwanda vinatokana na ile hali halisi ya watu kuyaona mazingira yao, wakaziona fursa, wakatatua shida zao kulingana na mazingira yao jinsi walivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sasa hivi ukiondoa hizo efforts zako unazozifanya kwenye viwanda, tengeneza timu maalum ya kufanya industrial mapping. Hiyo industrial mapping itanguliwe na research. Uwe na kitengo maalum kifanye tafiti eneo gani yanastawi mazao gani, eneo gani tukiweka kiwanda cha aina gani kitakwenda vizuri. Tukifanya hivi mambo yetu yatakwenda vizuri, bila kufanya research sasa na kujua ajenda ya viwanda si ajenda ya hiari. Hii ajenda ya viwanda ni ajenda ya lazima kwa sababu ndiyo National Agenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi leo tunasema Awamu ya Tano tuna ajenda gani, ni Tanzania ya viwanda hatuna ajenda nyingine. Sasa Tanzania ya viwanda ambayo hatuna mkakati wa viwanda, hatuwezi kwenda, uwe ni wimbo wa nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikupe mfano tu Tanzania tuna uzoefu wa kuamua na kufanikiwa. Mimi nina mifano miwili ambayo naijua kabisa tuliwahi kuamua na tukaenda. Siku tulipoamua kuweka standard gauge hatukuulizana na mtu tukaweka ikaenda. Siku tulipoamua kuifanya UDOM iwe university tukaamua tukaenda. Mimi nina imani mambo haya yote yanachohitaji ni kitu kimoja tu kuamua, kutenda na kutekeleza.