Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuchangia bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa mimi nianze kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa makusudi na dhati kubwa anayoifanya ya kuendeleza viwanda vya ndani. Anapambana kwa nguvu zake zote, na kweli Rais wetu ni mzalendo; na mimi niwaambie tu wale wanaobeza wanaosema hovyo, viwanda hivi siku vikija ku-achieve Magufuli atakuwa kamaliza muda wake, tutafaidika sisi, watoto na wajukuu zetu.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais anafanya kazi hii kwa ajili ya watanzania, ni wajibu wetu kumuunga mkono Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niungane na Wabunge waliotangulia kusema, lazima Serikali hii iwe na mkakati maalum. Tumechoka sasa kuagiza mara mafuta mara sukari, kama Mheshimiwa Rais anavyotaka viwanda vya ndani vifanye kazi basi na Waziri na viongozi wote wa Serikali waungane na Mheshimiwa Rais kwa vitendo. Tujiwekee labda miaka miwili au mitatu tusiagize tena mafuta wala sukari nje ya nchi, tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano sasa hivi NSSF wana shamba kubwa la miwa, ni kuhakikisha tunaongeza uwezo mkubwa kwa wafanyabiashara wengine wa viwanda, lakini NSSF tuweke nguvu zetu zote, wafanye bonde lingine na bonde lingine, tuwaongezee nguvu hatimaye miaka miwili tusinunue sukari nje ya nchi. Tuna uwezo mkubwa wa kufanya hivi kama tutaamua. Tuna Mkurugenzi mzuri sana pale NSSF mkimpa nguvu anaweza kufanya hili jambo, lazima tuwe na mikakati, lazima tuamue. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri Mkuu kwa kauli yake nzuri aliyoitoa juzi kuhusu sukari na mafuta, kwamba ndani ya siku tatu vitu hivyo viwe vimetoka. Nasema hivyo kwa sababu mahitaji ya mafuta ni tani 28 hadi 30 kwa mwezi, Januari, Februari na Machi tumeingiza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Aprili mafuta hayo waliyoleta nyaraka hazitimii, Serikali haiwezi kukuingizia bila nyaraka, hivi vitu ni mafuta/ni chakula, hauna TBS ya Malaysia tukuingizie kama, kuna sumu. Hakuna code iliyoonesha mafuta ghafi yamelipiwa Malaysia, Malaysia hawatoi mafuta ghafi bila kulipia kodi, nyaraka hazitoshelezi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii isiwe sababu ya kuwaadhibu Watanzania kwa kuficha mafuta haya. Nasema hivi nina maana yangu, haya mafuta waliyoingiza wanaita wameingiza crude oil (mafuta ghafi). Haya mafuta ghafi ya mwezi wa nne kwa mfano yangeingia mpaka process kila kitu labda tarehe nne au tano yangekuwa yameingia, lakini mafuta haya ni lazima waende kuya-refine kuyasafisha ili yaje kuingia sokoni. Mpaka waya-refine ina maana sokoni mafuta haya yangeingia kwenye tarehe 12, 13 na 14; leo vipi mafuta hakuna nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, watu hawa wameficha mafuta ku-demand bei ipande na kuikomesha Serikali. Nakupongeza sana Waziri Mkuu kwa kauli yako ya watoe mafuta, kwa sababu mafuta ya Aprili hata kama yangekuwa yameingia wangekuwa hawajamaliza kuya- refine, kuyasafisha na kuyaingiza sokoni, iwaje leo mafuta yapotee kabisa ndani ya soko la Tanzania. Mheshimiwa Waziri Mkuu mafuta yapo, Serikali iweke nguvu mafuta yatoke na Watanzania wauziwe kwa bei inayostahili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa tuamue kabisa, tuna asilimia 30 ya mafuta tunayolima mbegu hapa Tanzania, tuamue kuwekeza. Serikali juzi iliamua kuwekeza nguvu zake zote kwenye pamba, TAMISEMI, Waziri wa Viwanda, Waziri wa Kilimo, Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya hatimaye mwaka huu pamba imekuwa nyingi sana Mwanza. Tuamue kwenye alizeti, michikichi. Hatuwezi kuamua kwenye vitu vyote kwa wakati mmoja, tuchague mazao yetu ambayo tuamue, kwa mfano uchukue Dodoma, Singida, Tabora useme ni zone ya alizeti, hii ni zone ya alizeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwijage nimepitia hotuba yako kuna sehemu umesema una matrekta 148 unauza, nikwambie kwa hali ya sasa hivi kununua cash yale matrekta watu wengi hawatamudu. Sasa lazima Serikali itusaidie. Mimi niombe tuanzie Mkoa wangu wa Tabora, nina wilaya saba, kila Halmashauri moja mtupelekee matrekta matatu mtukopeshe, mdhamini atakuwa Halmashauri, Mkuu wa Mkoa, DC na mimi Mbunge wa Viti Maalum pamoja na Wabunge wa Majimbo yangu ya Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapewe matrekta matatu matatu, haya matrekta yawe mali ya Halmashauri, mtu akienda Halmashauri aandikiwe mkataba utajaza mafuta, utalipa posho, ukiimbua utalipa pesa za gharama ya kulimia. Zile pesa zitakuja kulipwa kwako Mwijage, lakini hutapata cash lakini utakuwa umesaidia Watanzania. Wakati huo huo mtafute mbegu za kisasa za alizeti, zilizopo hazitoi mafuta mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwijage hata mchikichi pia tufanye vivyo hivyo. Mchikichi unaweza kupeleka Kigoma, Mbeya kwa maana ya Kyela pamoja na Katavi na ukaita mchikichi zone na akili zote, viongozi wote wakaelekezea kwenye haya mambo, inawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumechoka kunyanyasika Mheshimiwa Mwijage, watu wanaficha mafuta demand inapanda, Serikali nzima inapata stress mnashindwa kufanya vikao na vitu vingine, mnakaa kwenye vikao mpaka saa saba za usiku, hivi vitu tunaviweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbona Rais ameamua tutajenga standard gauge, Afrika nzima hakuna anayejenga standard gauge kwa hela yake, mbona ameweza? Mbona ameamua kununua ndege na kusomesha elimu bure ameweza; watu wamepiga kelele haiwezekani, imewezakana. Nina amini tukifanya hii alizeti zone na mchikichi zone tukawekeza tunaweza Mheshimiwa Mwijage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi trekta zikipelekwa Halmashauri wakabidhiwe wakurugenzi ma-DC, RC na Wabunge watu wakakope pale kwa mikataba wakalime baadae watalipa kwenye Halmashauri, tutaenda mbali sana. Pia mtusaidie viwanda vidogo vya kukamulia hizi alizeti, kila Halmashauri ikopeshwe. Serikali bado ina uwezo huo, Halmashauri zetu zina uwezo wa kununua viwanda vidogo, ni maelekezo tu. Kama kweli tumeamua kumsaidia na kumuunga mkono Mheshimiwa Rais naamini hivi vitu vinawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee sasa kuhusu suala zima la viwanda, nianze na Kiwanda cha Tabora. Tabora kule tuna kiwanda cha nyuzi, kiwanda cha nyuzi cha Tabora kinazalisha pamba, tumekuja kuomba mara kadhaa pamoja na mwenye kiwanda tuiombe Serikali inunue pamba za hospitali kutoka kwenye kiwanda cha nyuzi cha Tabora; tuwasaidie wenye viwanda vyetu, kwa mfano mtu ana kiwanda cha kutengeneza kitu ambacho kinawezekana Serikali kinaitaka, Serikali inunue kwake kumpa support. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais kila siku amekuwa akisema jamani tengenezeni hata syringe za hospitali tutanunua kwenu, kwa hiyo tum-support. Kule Tabora hamji kununua pamba kwa ajili ya matumizi ya hospitali, mnaagiza nje ya nchi. Tunaomba Mheshimiwa Mwijage mje mnunue kule kwetu Tabora. (Makofi/kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niendelee kuongelea viwanda vidogo, kumekuwa na kebehi zinafanyika hapa Bungeni kwamba cherehani si viwanda, hakuna viwanda 3000; mimi naomba ni-declare kuhusu cherehani, nitoe ushuhuda. Kuna ndugu yangu ni fundi cherehani, alishindwa
kusoma akaishia form three akajisomesha cherehani akaendelea akanunua cherehani nne, huyu akaenda kukopa benki, wakamwambia huwezi kukopeshwa bila leseni wala TIN, akapata. Baadae akapata tender ya kutengeneza mashati ya taasisi X, siwezi kuitaja hapa, wakamlipa shilingi milioni 70; sasa hivi amenunua cherehani 45. Mheshimiwa Mwijage nifuate nitakuonyesha na amenifuata mimi, dada nitafutie eti tenda ya kushona nguo za jeshi nikamwambia eeh umefikia huko mwenzetu? Kwa hiyo, wale wanaodharau hizi cherehani nawaambieni hivi watu wanatoka kwa hizi cherehani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe sasa Serikali kwa sababu Serikali mmekubali cherehani ni viwanda vidogo hakikisheni taasisi zenu, wenye viwanda hivi vya cherehani wapeni kazi. Kwa mfano uniform za TPA, TANAPA na uniform sijui za nini wapeni washone, wapeni uwezo, watu wasiende kushona hizi uniform nje, Serikali hii inaweza ni kiasi cha kujipanga tu. Kwa hiyo, mimi bado naitia moyo Serikali kwamba tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, A to Z ya Arusha ni kiwanda kikubwa sana, Kamati tuliwahi kwenda kutembelea mwaka 2013. Historia yake mwenye A to Z alikuwa na cherehani moja, alianza na cherehani moja, mwenye A to Z ya Arusha, anayebisha akamuulize. Leo hii ni kiwanda kikubwa duniani, hata huu mchakato wa malaria amepata tender viwanda vitano duniani na yeye amepata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, anatengeneza mashuka, uniform na kila kitu. Kwa hiyo, tusidharau hizi cherehani watu wanaponda viwanda gani kama cherehani, mimi nasema hivi ni viwanda na vinafanya kazi na watu wananufaika kutokana na hizi cherehani.