Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nitumie nafasi hii kwanza kusema mambo machache; mwaka 2016 wakati tunachangia bajeti ya kwanza ya Wizara ya Viwanda na Biashara nakumbuka nilimwambia kaka yangu Mheshimiwa Mwijage kwamba nasubiri nione muujiza na nilitaja miujiza ambayo nilikuwa naisubiri na leo haijatokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muujiza wa kwanza niliokuwa nausubiri ni kuona namna gani Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji inaweza kuunganisha mambo matatu ambayo Waziri amekabidhiwa. Mheshimiwa Rais alivyokuja na vision ya ku-revive industrialization aliamua kwa makusudi kuunganisha biashara, uwekezaji na viwanda ili kuweza kufikia lengo la industrialization.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka leo bado tunazungumzia General Tyre, mpaka leo tunazungumzia Liganga na Mchuchuma, mpaka leo tunaongelea matatizo ya msingi ya biashara na huoni yakijadiliwa katika hotuba za Waziri na hata kwenye mpango wetu wa mwaka mmoja, miwili na huu ni wa tatu. Tusome ukurasa wa 138 wa hotuba ya Waziri. Waziri ametaja vipaumbele na malengo ya mwaka 2018/2019. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri ametaja vipaumbele kushirikiana na taasisi kutunisha mtaji wa NEDP, kuendeleza miradi ya kieleleza ya Mchuchuma na Liganga, Engaruka Kiwanda cha Matairi, utekelezaji wa eneo la TAMCO, mradi wa kuunganisha matrekta, uendelezaji wa maeneo ya viwanda ya SIDO. This is a hundred percent kwa miaka mitatu tunajadili the hardware part of business, hatujadili the software part of the business. Ili tuweze kuona matatizo tuliyonayo kwenye software part of the business naomba nitaje haya mambo. The software part of business ni regulations na sheria na mfumo wetu wa kodi, huu ndiyo utachochea haya mambo mengine yote kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania katika kufanya biashara according to the World Bank Report ni ya 137 kati ya nchi 190 katika mazingira ya kufanyia biashara, Tanzania ili uanzishe biashara ni nchi ya 162 kati ya nchi 190; Tanzania ni ya 150 kwa ajili ya kutoa vibali vya kufanyia biashara. Kama kweli tunataka ku-break through ni lazima Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha wakae kwa pamoja kwa ajili ya kutengeneza the softaware part ya kufanya biashara katika nchi, tusipofanya namna hii tutakuja hapa tutaimba kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano wa leather sector; na ndugu yangu Mheshimiwa Mgumba, ameongelea Kiwanda cha Ngozi cha Morogoro. Kwa takwimu kwa mwaka sisi tunazalisha vipande milioni tatu vya ngozi katika nchi. Sasa ili kiwanda chetu cha ngozi kiweze kuzalisha, na nimeona kwenye mpango tunatenga 10 billion kwa ajili ya kuandaa eneo la viwanda vya ngozi, tuna viwanda saba ama vinane havifanyi kazi, halafu tunataka kutenga bilioni kumi nyingine kwa ajili ya kuandaa eneo la viwanda hapa nchini, this is wastage of resources. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikupe mfano, katika uzalishaji wa leather sector tuna-process ngozi kutoka katika hatua ya raw material kwenda kwenye wet blue, kutoka wet blue kwenda kwenye crust na kutoka kwenye crust kwenda kwenye finished, hizi ni levels tatu. Level ya kwanza investment inayohitajika kwa kiwanda cha kati ni 15 million US dollars; kutoa kwenye wet blue kwenda kwenye second level ambayo ni crust unahitaji five million dollars; kutoka kwenye crust kwenye level ya finished unahitaji another five million dollars, this is 25 million dollars. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini angalia kodi za mzigo. Ukizalisha wet blue ili ui-export kwenda nje unalipa ten percent export levy, unalipa wharfage dola 40, unalipa MoFED dola 100 halafu uki-import chemicals unalipa dola 190 kwa ajili ya import duty, lakini bado utalipa 18 percent VAT. Huyu mtu atahitaji apate chemical permit, alipe dola 667, atalipa railway development levy ya 1.5, atalipa, wanaita corridor levy ya 4.9 dollars; lakini bado ana Government taxes, kuna workers’ compensation, kuna municipal levy, kuna tax, kuna Government chemistry fee, kuna OSHA, NEMC, other crises.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hebu compare leather sector na nchi zilizotuzunguka; hakuna export duty ya 10 percent ya wet blue ukienda Kenya na Uganda. Halafu ngozi zetu zinazozalishwa ndani ya nchi huyu mwenye kiwanda hawezi ku-process kwa sababu atakapozalisha kwenda kuuza nje, the cost of processing wet blue square feet moja ni dola 30, na soko la dunia ni dola 30 anauza wapi? Hata tujenge viwanda milioni we cannot. Ni lazima Serikali itambue kwamba number one principle ya biashara ni kutengeneza mazingira condusive ya watu wetu waweze kuzalisha at a competitive rate. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano mwingine, nchi ambayo ilifungua soko lake pamoja na sisi ni Vietnam na Waziri ameshawahi kwenda mwaka 1986. Na Waheshimiwa Wabunge tuelewe, viwanda ni vya aina tatu; tunazungumzia manufacturing, processing and assembling, hivi ndivyo viwanda tunavyovizungumzia. Manufacturing and processing kuna technological advancement kila siku, leo tunazungumzia textile industry, je, tuna raw material ya kutosha kulisha viwanda vyetu tulivyonavyo? Je, tumeweka mpango gani wa ku-invest katika uzalishaji wa raw material? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunazungumzia mafuta, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, kwa mwaka tunatumia dola milioni 240 ku-import mafuta ya kula katika nchi yetu. Lakini tunahitaji shilingi ngapi kuondoa hili tatizo? Mpango uliopo kwenye African Development Bank wa African Edible Oil ili sisi tuondokane na importation ya mafuta ya kula katika nchi we only need 45 million US dollars ili tuweze kulima michikichi ambayo tutazalisha mafuta, tutaondokana na tatizo la ku-import mafuta, where is the plan? Hakuna! Hela ipo kwenye ADB, ni accessible.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani, Dkt. Magufuli ataimba, ndiyo maana kila siku anabadilisha sheria huko State House, because the old man is frustrated. Anaongea hivi it seems like yeye yuko mbingu ya saba wengine tuko kwenye ardhi, what is the problem? Wizara ya Viwanda na
Biashara what is the problem? Wizara ya Fedha what is the problem? Wizara ya Kilimo what is the problem? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia hapa ndugu yangu Mheshimiwa Ulega anazungumzia exportation ya nyama. 70 percent ya ngozi tunayoizalisha katika nchi yetu ni grades four, five, six and seven, hatuna ngozi ya grades one, two wala three katika nchi yetu. Why? Because hatujafanya proper breeding ya mifugo. Hakuna mpango, Wizara ya Mifugo ukisoma huu mpango wa mwaka mmoja Waheshimiwa Wabunge Serikali inapanga eti kutafuta madume kumi ya kupanda ng’ombe, hivi mnajua madume kumi ni shilingi ngapi, ni 20 million shillings, this is the plan, it is here, iko humu kwenye mpango. There is no seriousness. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.