Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuchangia machache. Kwanza ningependa kusema kwamba Serikali kama ina mpango mkakati wa kuhakikisha sekta hii ya viwanda inafanya kazi vizuri, ningependa ifahamu kwamba kilimo kiwe ni kipaumbele kwa ajili ya kulisha viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ningependa kuzungumzia kwa vile nina muda mchache ningependa kuzungumzia biashara kwa ujumla nikianzia na TRA. TRA imekuwa ni tatizo kwa sababu unapotaka kupata TIN kwa mfano TRA, utaenda kama unatafuta kazi, kwanza wafanyakazi wa TRA ni wachache, ilitokea tangazo hapa wafanyakazi wanaotakiwa kuajiriwa 400 na zikatokea nafasi 56 wakaomba. Wale 400 hatujui kama wameajiriwa au hawajaajiriwa. Wengine wanasema mpaka sasa hivi hawajaajiriwa. Imesababisha TRA kuwa na upungufu wa wafanyakazi na hivyo wananchi kupata shida sana kupata mahitaji yao pale TRA. Kwa hiyo, TRA imekuwa na usumbufu mkubwa sana. Kwa hiyo, naomba Serikali ifanye mchakato wa kuongeza wafanyakazi ili TRA iweze kufanya kazi kama inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kusema kwamba biashara ni matangazo. Nimeona viwanda kwa mfano kuna Kiwanda pale Kibaha cha Viuatilifu. Tangu uzinduzi umefanyika hamna mtu hata wa Kibaha anayejua kiwanda kile kinafanya kazi gani, kwa sababu hamna uzalishaji, hamna biashara kimekaa kama pambo. Tulitarajia watu wa Kibaha kwamba kiwanda kile kikiwepo vijana wetu watapata kazi, lakini kinyume cha hapo ni kwamba kile kiwanda hakifanyi kazi inayotakiwa na biashara ya viuatilifu hatuioni. Na matangazo ya kuonesha kwamba labda kiwanda kile kipo pale kwa sababu kina faida fulani hamna, hamna matangazo yanayoonesha kwamba wananchi wanaweza wakapata hizo dawa labda hata za majumbani kuondoa mazalia ya mbu, hatuoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ningependa kumwambia Waziri hivi viwanda vinavyoaanzishwa basi na matangazo yawepo. Viwanda visaidiwe kufanya matangazo, viwanda vimekaa kama picha hamna kinachoendelea. Pale Kibaha kuna matrekta tunayaona hatujui yapo pale kwa ajili ya nini kwa sababu wananchi hawajatangazia kwamba aidha yale yanauzwa au chochote, sasa biashara za viwanda kama hazitaenda na matangazo ina maana ni sawa sawa na kutwanga maji kwenye kinu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kusema kwamba Tanzania tunashindwa kufanya biashara ya ku- export, wananchi wengi wanashindwa kwa sababu Serikali haijatoa elimu juu ya ufungashaji. Unakuta kwamba mazao yanazalishwa hapa halafu yanachukuliwa yanapelekwa Kenya, wanafanya ufungashaji kupeleka nje na yanakuwa labeled kwamba mazao haya yanazalishwa Kenya. Sasa kama Tanzania tunataka kufanya biashara basi eneo la ufungashaji liboreshwe ili wananchi wajue akiwa na bidhaa yake anaifungasha vipi ili aweze kuipeleka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia eneo la biashara za nje kuna usumbufu na urasimu mkubwa sana kiasi kwamba watu wakitaka kuuza bidhaa zao nje wanapata usumbufu kiasi kwamba wanakata tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuuongelea juu ya wasindikaji wadogo, wamekata tamaa walio wengi kwa sababu kwa ajili ya zile tozo ambazo ni msululu. Unakuta kuna TFDA, kuna OSHA, kuna TBS kibiashara chenyewe ni kidogo production ni ndogo product moja unavyotaka kwa mfano ya spice anataka kutengeneza viungo unakuta kwamba msululu wa kodi zenyewe zilizoko pale zinamfanya huyu mjasiriamali mdogo ashindwe kufanya uzalishaji. Kama tunataka viwanda vidogo kama tulivyosema kwamba hata anayetwanga tangawizi yake akai-pack anaweza kuwa ni kiwanda basi hizo kodi tupunguze ili viwanda vidogo hivi viweze kumudu gharama hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti ningependa kuongelea juu ya ukaguzi wa Idara ya Viwandani. Tumefurahi kweli viwanda vimekuja watoto wetu waweze kupata kazi lakini wanapata magonjwa kuliko hata kazi wanayofanya. Kwa sababu unakuta kwamba viwanda havina vitendea kazi mtu anafungasha pale Kibaha kuna Kiwanda cha Sabuni. Siku nzima anabeba sabuni zile, anahamisha, anafungasha lakini hata kinga yake hana. Hana hata ile mask ili ya kufunga puani ili angalau asivute yale mavumbi.