Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tozo mpya imeibuka mpakani Tunduma inaitwa tozo ya uzito wa mizigo inayotokea Zambia ambapo lori moja hulipishwa hadi shilingi 400,000. Hii ni kero mpya na inachangia kuongeza gharama za uzalishaji kwa viwanda vya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni hili la Kurasini Logistic Centre. Natambua jitihada binafsi za Mheshimiwa Waziri lakini sina budi kuliingiza katika rekodi ili nguvu iongezeke katika kulishughulikia suala hili hasa ukizingatia pesa nyingi ya Serikali iliyoingia hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu la mwisho ni unyanyasaji wa TRA dhidi ya wafanyabiashara kwa kuwakadiria kodi kubwa kuliko hata mitaji yao kimakosa na wanapotakiwa kuhakiki inachukua muda mrefu sana na kuathiri uzalishaji.