Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namkushukuru Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa hotuba yako nzuri, napenda kupongeza Kamati ya Viwanda na Uwekezaji kwa maoni yao, naomba Serikali iyafanyie kazi maoni hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi ushauri wangu katika Wizara hii naomba katika Mkoa wangu wa Kagera tupatiwe viwanda vidogo vidogo, tunalima maparachichi kwa wingi yanaharibika mashambani, nanasi zinastawi sehemu nyingi, hata ndizi zinaweza kukaushwa na kuwa- packed katika mifuko ya plastiki, tukitumia utaalamu tutapata hela za kujikimu shida zetu. Mkoa wa Kagera ni wa mwisho kwa umaskini au ni wa pili kutoka mwisho, Mheshimiwa Waziri ikupendeze utuonee huruma walau tufikirie tuwekwe kwenye list ya watakaofikiriwa kuanzishiwa viwanda vidogo vidogo na vya kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawatakia kazi nzuri na ya mafanikio, Mungu awabariki sana.