Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji Wakuu kwa kazi nzuri inayofanyika katika Wizara ya Viwanda na Biashara. Wengi hawakuamini kuwa Tanzania ya viwanda inawezekana hayawi, hayawi, sasa yamekuwa. Nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa viwanda vingi ambavyo vimeanzishwa nchini, viwanda hivi ndivyo vitaipeleka nchi yetu kwenye uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wengi wamehamasika kuanzisha viwanda, wanachohitaji ni kuwa karibu nao ili wapate ushauri wa kina. Wanahitaji ushauri/elimu juu ya aina ya viwanda vinavyofaa kuanzishwa katika maeneo yao, viwanda vitakavyotumia malighafi zinazopatikana karibu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawa wanahitaji ushauri wa kitaalam wa hatua za kufuata katika kuanzisha kiwanda (usajili, tozo, kodi, uthibiti na kadhalika) watu hawa wangependa kupata ushauri wa kitaalam wa namna ya kupata masoko. Wanahitaji kujua wapi mitaji rahisi inapatikana. Mheshimiwa Waziri aliwahi kusema kuwa upo mwongozo wa namna ya kuanzisha viwanda, tunaomba huo mwongozo usambazwe na wengi wausome.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mikoa mingi imeanza kupiga hatua kwa sababu wapo wafanyabiashara wengi wamewekeza kwenye Mikoa hiyo. Mkoa wa Kagera utaendelea kubaki nyuma sababu uwekezaji Mkoani wa Kagera uko chini sana, chini ya asilimia mbili. Wawekezaji wengi wanauona kuwa Mkoa wa Kagera uko pembezoni, uko mbali na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha wawekezaji ili wakubali kuja wengi kuwekeza Mkoani Kagera?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.