Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa jitihada zake za makusudi za kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iendelee na mikutano ya mara kwa mara na wadau, wawekezaji na wafanyabiashara ili kubaini changamoto, matatizo na vikwazo vinavyowakabili ikiwemo kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendeleza sekta ya viwanda ni lazima kuiendeleza sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo vipewe kipaumbele ili kupata malighafi za kupeleka viwandani, malighafi zitoke hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wa viwanda vya maziwa wana changamoto ya kodi mbalimbali hivyo ni vema eneo hilo liangaliwe upya. Wafanyabiashara wadogo wadogo kama mama lishe na wajasiriamali wadogo wanasumbuliwa sana kuhusu kodi, hawana uwezo wa kulipa kutokana na faida kuwa ndogo. Serikali iangalie jambo hili ili wananchi wetu wanyonge waweze kujikwamua na umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.