Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote wa Wizara kwa jinsi wanavyojituma katika jitihada ya kuusimamia na kuutekeleza kwa vitendo uchumi wa viwanda nchini, pamoja na changamoto zote na utofauti wa uelewa wa nini ni kiwanda kwa wananchi, baadhi ya wenzetu wa upande wa pili, ni vema yakatolewa maelezo ya ufafanuzi kwa lugha nyepesi ya nini ni kiwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa wananchi wanashughulika wao wenyewe bila ya kusukumwa katika shughuli za kilimo mahindi, mpunga, maharage, ulezi, alizeti, miwa, ufuta na kadhalika. Utaratibu wa kuuza mahindi nje ya nchi, natoa ushauri Serikali kutoa kiasi maalumu na kiasi kikubwa yaongezwe thamani (unga) wa kuuzwa huko. Kuongeza pato kwa mkulima na Taifa letu, mfano asilimia 25 kwa asilimia 75 au asilimia 45 kwa asilimia 55 kwa kuanzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maelezo mema yaliyofuatia zoezi la wafanyabiashara ndogo ndogo kutengewa maeneo katika ukurasa 43 - 44 ndani ya hotuba ya Waziri kwa mikoa minne kati ya 26 hii kasi ndogo, kwani wafanyabiashara ndogo ndogo ni eneo pana kwa vijana wetu la kujiajiri, hivyo tunahitaji kuongeza kasi, kwani tutawakatisha tamaa vijana na kusababisha wakajiunga na mambo yasiyostahiki kwao na Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali/Wizara kufuatilia zoezi hili ndani ya muda wa miezi sita ya mwaka 2018/2019 kwani ni kero iliyokithiri ndani ya nchi kwa hawa wafanyabiashara ndogo ndogo na ni sehemu kubwa ya wapiga kura wetu ili tuachane na hii changamoto. Pia Serikali
kuangalia namna sahihi na rafiki kwa wafanyabiashara kuhusu na malipo ya VAT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa 29 - 30 wa hotuba inazungumzia suala la usindikaji wa mafuta ya alizeti ingawa tuna pamba, karanga, ufuta na kadhalika, kwa mchanganuo wa hizi mbegu zitolewazo mafuta, ndiyo asilimia 30 ndani ya hayo mahitaji yetu ya tani 700,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuona umuhimu wa dhati na kulegeza masharti kwa viwanda vya mafuta ya pamba na alizeti ambayo tunayatumia sana nchini kuongeza idadi ya viwanda kutoka 21 na kuongeza idadi ya viwanda vidogo kutoka 750 kwa kuweka lengo hadi tufikapo mwaka 2020 tufikie uzalishaji wa asilimia 45 ya mafuta ya kula, kwani mazao hayo yanazalishwa kwa wingi hapa nchini ni kuwaongezea uwezo wa kilimo bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuweka mkazo kwa wafanyabiashara wote watakaohusika kwa namna moja au nyingine yaani chakula, mafuta na sukari kwa ndugu zetu wa Kiislamu ili waweze kutimiza ibada ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.